DAR ES SALAAM: Msanii wa Bongo fleva nchini Omary Nyembo, ‘Ommy Dimpoz’ ameungana na watanzania wapenda shampeni barani Afrika kuadhimisha siku ya Shampeni Duniani.
Akizungumza na habari leo Ommy Dimpoz amesema amefurahia kupata nafasi ya kujumuika na mashabiki zake.
“Nimefurahia kujumuika na mashabiki zangu katika kusheherekea siku ya shampeni duniani.”
Sherehe hii ya kupendeza iliangazia shampeni bora zaidi duniani, Moët & Chandon, inayosifika kwa utamaduni wake wa karne nyingi wa utengenezaji mvinyo wa kipekee, uliojawa ufundi wa hali ya juu kutokana na matengenezo yake maridadi zaidi kuwahi kutokea.
Sherehe ya Siku ya Shampeni ya mwaka huu ilikuwa ya kipekee sana kwani iliadhimisha kumbukumbu ya miaka 280 ya moetchandon tangu kuanzishwa kwake huko Epernay, Ufaransa, mwaja 1743.
Siku ya Shampeni na kukumbatia mila na ustaarabu ambao Moët & Chandon huleta katika nyakati bora zaidi za maisha.
Kwa upande wake, George Williams, mmiliki wa “Style Your Soul,” anatoa mtazamo tofauti wa Kitanzania. Na mialiko kwa marafiki wenye ushawishi katika tasnia na mtindo wa maisha, na kudai sherehe hiyo ni moja ya nyakati bora za maisha.
Kivutio kikuu cha ziara ya Williams kilikuwa uchunguzi wa mpango wa kilimo wa Moët & Chandon, ‘Natura Nostra.’ Mpango huu, ulio mstari wa mbele katika kilimo cha miti shamba, ni ushuhuda wa kujitolea kwa Moët & Chandon katika kuhifadhi mazingira. ‘Natura Nostra’ imejitolea kusaidia bayoanuwai na kulinda mimea na wanyama wa ndani katika eneo la kilimo cha bidhaa ya shampeni.
Aimee Kellen, Mkuu wa Ushirikiano wa Watumiaji wa Moët Hennessy Afrika na Mashariki ya Kati, alieleza, “Siku ya Champagne ni fursa ya kusherehekea urithi wetu wa kuchagiza tasnia na kushiriki juhudi zetu za uendelevu na Afrika na ulimwengu.”