Simba kazi imeanza upyaaa

DAR ES SALAAM: MENEJA Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba, Ahmed Ali amesema kuna kazi kubwa ya kupita tawi kwa tawi kurudisha hamasa kwa mashabiki wa Simba.
Ameyasema hayo katika Mkutano wake na waandishi wa habari kuelekea mchezo wa kuwakabili Asec Mimosas ya Ivory Coast katika hatua ya makundi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Novemba 25, 2023 Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.
“Mechi hii ukisinzia tu unapata watu wachache uwanjani. Mashabiki hamasa yao ipo chini. Niwaambie mashabiki, njoo na hasira zako, furaha utaikuta uwanjani,” amesema Ahmed Ali
Meneja huyo amewaomba mashabiki wa klabu hiyo kuiunga mkono timu yao, wakati huu uongozi ukiendelea kuimarisha benchi la ufundi kwa kusainisha makocha wenye viwango.
Kuelekea katika mchezo huo, Ali amesema kauli mbiu ni ‘Twendeni Kinyama (Kisimba simba), Mashabiki Bomba’.
I’m making more than $75k by just doing very easy and simple online job from home. Last month my friend sis received $94,380 from this work by just giving only 2 to 3 hrs a day. Everybody start earning money online.
.
.
Detail Here————————————————–>>> http://Www.BizWork1.Com
Thanks for the info, just started this 4 weeks ago. I’ve got my FIRST check total of $350, pretty cooll.!
Work At Home Special Report! (financereports.online)