Simba kubaki na silaha zake

KLABU ya Simba imesema hakuna mchezaji ambaye yupo kwenye mipango ya yao atakayeondoka msimu huu.

Meneja wa Habari na Mawasilino wa Simba, Ahmed Ally amesema uvumi wa Simba kuachia baadhi ya wachezaji msimu huu akiwemo Mohammed Hussein, Baleke na Manula hauna ukweli.

“Niwathibitishie wana Simba hakuna mchezaji ambaye yupo kwenye mipango yetu ataondoka.”amesema Ahmed Ally.

Advertisement

Ameongeza kuwa wachezaji waliomaliza mkataba ambao watatakiwa kuendelea watafanyiwa maboresho kwa lengo la kubaki nao.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *