Simba SC ruksa kusajili

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Ulimwenguni (FIFA) limeondoa adhabu ya kutosajili kwa klabu ya Simba SC baada ya kukamilisha madai ya fedha ya usajili ya klabu ya Teungueth kuhusu usajili wa Pape Sakho.

Awali, Simba ilifungiwa kusajili baada ya kushindwa kuilipa klabu hiyo kutokana na mauzo ya Sakho.

Baada ya kukamilisha malipo hayo, Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) pia limeifungulia Simba kusajili wachezaji wa ndani.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *