Simba wawafariji mashabiki

Simba wawafariji mashabiki

NAHODHA wa Simba, John Bocco amewaomba msamaha mashabiki wa klabu hiyo kufuatia matokeo ya sare ya bao 1-1 waliyoyapata jana usiku katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Namungo FC mchezo uliofanyika Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.

Akizungumza na HabariLEO, nahodha huyo amekiri kuwa matokeo hayo yamefifisha matumaini yao ya kufukuzia ubingwa hasa kama wapinzani wao Yanga watashinda mchezo wa leo dhidi ya Singida Big Stars.

“Ni matokeo ambayo hata sisi wachezaji hatukuyategemea na yametumiiza pia,   ndio maana kwa niaba ya wachezaji wenzangu tunaomba msamaha tutahakikisha tunapambana ili kushinda mechi tatu zilizobakia na kupigania ubingwa wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), ili kuwapa furaha mashabiki wetu,” amesema Bocco

Advertisement

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *