Simba yashusha kifaa kutoka Cameroon

Simba SC imetangaza kumsajili beki wa Kimataifa wa Cameroon, Che Fondoh Malone (24) kutokea klabu ya Cotton Sport ya nchini humo.
Che Malone ambaye ni mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Ligi Kuu Cameroon msimuwa 2022/2023, amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba SC.
Usijali huo ni watatu kwa Simba, kwani tayari imemsajili, Willy Essomba na Aubin Kramo.