Steve Nyerere: Watanzania tuwashike mkono waathirika wa Hanang

DAR ES SALAAM: Mwenyekiti  wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Mengele ‘Steve Nyerere’ amewaomba watanzania kuwachangia huduma za vitu mbali mbali waathirika wa mafuriko Hanang.

Akizungumza na waandishi wa habari juu ya Programu ya Mama amstiri Mwanamke jijini Dar es Salaam Steve Nyerere amesema kuwa taasisi hiyo imelenga kutoa taulo kwa Wanawake 200,00 sambamba na kutoa miswaki na nguo za ndani.

“Tumekuwa tukichangia harusi na kutoa zawadi na kufanya Birthday lakini tumelisahau kundi la watu waliopata matatizo.”amesema Steve Nyerere.

Advertisement

Steve Nyerere amesema unavyoweza kusherekea sikukuu unahitaji kujua kuna jamii kundi la wanawake wapo Hanang wanahitaji furaha kutoka kwako kupewa kipaumbele katika kulisaidia kundi hilo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *