TADB waomba kibali kufungua kiwanda

BENKI ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), imetuma ombi kwa serikali la kutoa kibali kwa mwekezaji cha kufungua Kiwanda cha kuchakata korosho katika Kanda ya Kusini.
Akitoa ombi hilo mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, leo Julai 6,2023 katika uzinduzi wa ofisi ya benki hiyo Kanda ya Kusini, Mkurugenzi wa TADB Frank Nyabundege amesema iwapo serikali itatoa kibali, kitajengwa kiwanda cha kuchakata korosho kuanzia kwenye kubangua korosho ghafi (RCN), kuzisafisha mpaka kuzifungia kwenye vifungashio na kuzisafirisha nje ya nchi.
Amesema, Kiwanda hicho kinatarajiwa kutoa ajira zaidi ya 1,800 ambazo kati ya hizo asilimia 90 itakua ni wanawake.
“Kiwanda hiki kitakua na uwezo wa kubangua tani 33,000 kwa mwaka na kitaanzisha miradi ya mfano ya kina mama takribani 500 ambao watakopeshwa mashine ndogo ndogo za kubangua na kuchakata korosho na kuzipeleka katika nchi za Marekani na Ujerumani, ” amesema na kuongeza:
“Mh Waziri Mkuu, naomba nimtaje mwekezaji huyu ambaye ni mwanamke mzalendo na mfanyabiashara mashuhuri Sarah Masasi ambae anategemea kuweka kiwanda cha kisasa chenye teknolojia ya kusafisha korosho katika viwango vya kimataifa mkoani Lindi.
“Tunapopata wawekezaji kama hawa, sisi kama Benki ya Maendeleo tupo tayari kuchagiza mabadiliko katika sekta ya kilimo.”
Amesema, TADB kwenye mnyororo wa thamani wa korosho katika Kanda ya Kusini wamekopesha sh bilioni 35 tangu msimu wa mwaka 2018/2019.
“Mh Waziri Mkuu, tunafahamu kuwa Kanda ya Kusini ni kanda ambayo wakulima wake wamejikita katika kilimo cha zao la korosho, kwa kutambua hilo, sisi kama benki tumelipa kipaumbele zao hili ndio maana tunawekeza fedha nyingi katika zao hilo,”amesema.
Finalement, j’ai fait 145 $/h. Il est temps de passer à l’action et vous pouvez également le rejoindre. C’est un moyen simple, dévoué et facile de devenir riche. Dans trois semaines, vous souhaiterez avoir commencé aujourd’hui. Essayez-le simplement sur le site d’accompagnement.
BONNE CHANCE…. https://onlineweb76.blogspot.com/
Stay at home mom Kelly Richards from New York after resigning from her full time job managed to average from $6000-$8000 a month from freelancing at home
This is how she did it… https://fastinccome.blogspot.com/
I getting Paid upto $18953 in the week, working on-line at home. I’m full time Student. I shocked when my sister’s told me about her check that was $97k. It’s very easy to do. everybody will get this job.Go to home media tab for additional details.
See—->>> http://Www.Easywork7.com
Working part-time and making an extra $15,000 or more online is a simple and quick method to gain money. I earned $17,00 in the preceding month by working in my spare time, and I am incredibly grateful for this opportunity.
.
.
Details Here——————————————————>>> http://Www.OnlineCash1.Com