WAZIRI Mkuu wa Australia, Tony Abbot amempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuamua kukabidhi madaraka kwa kiongozi mwingine kwa mujibu wa Katiba nchini Tanzania. Baada ya kuitumikia nchi kwa miaka 10 kuanzia mwaka 2005, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kukabidhi madaraka kwa Rais wa Awamu ya Tano mara baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
zaidi ya miaka 5 iliyopita
BAADA ya miaka 38 ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kada wake maarufu, Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amejitoa na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
CHUO Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kinaratibu mradi wa utafiti wa kusaidia kuzuia kuoza kwa matunda yanayozalishwa nchini ili kuhimili katika masoko mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.
MWENYEKITI wa Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Hamisi Msumi ameahirisha kusikiliza shauri linalomkabili Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge la kupokea kiasi cha Sh bilioni 1.6 kutoka kwa kampuni ya VIP Engineering hadi Agosti 6, mwaka huu baada ya mbunge huyo kutuma maombi.
MAOFISA ambao ni vijana nchini wametakiwa kutumia elimu wanayopata katika kuwaendeleza vijana kiuchumi ili kuwawezesha kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali.
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco), limesema litaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kuhakikisha kwamba taifa linakuwa na wananchi wenye uwezo mkubwa wa kuvumbua kwa kutumia Elimu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama).
JUMUIYA ya Wanawake ya Chama Cha Mapinduzi (UWT) imechangisha zaidi ya Sh milioni 722 katika harambee iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana.
SERIKALI imeongeza muda wa mwisho wa kukamilisha ukusanyaji wa takwimu za Sensa ya Viwanda kote nchini hadi Agosti 31 mwaka huu, kutokana na viwanda 366 vilivyoko Dar es Salaam kushindwa kuwasilisha taarifa muhimu za uzalishaji kwenye madodoso ya sensa hiyo.
NAIBU Kamishna Kitengo cha Upelelezi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Loicy Apollo, amekiri kupokea kiasi cha Sh milioni 80.8 kutoka kwa James Rugemalira, na kufafanua kuwa alipatiwa kiasi hicho kama mkopo usio na riba wa matibabu na biashara.
ALIYEKUWA Mbunge wa Viti Maalumu, Leticia Nyerere (Chadema) amesema ametua mzigo mzito wa miaka mitano baada ya kutangaza rasmi kurudi Chama Cha Mapinduzi (CCM).