SERIKALI imepongezwa kwa kutambua juhudi zinazofanywa na wasanii, wanamichezo na waandishi wa habari za kujenga nyumba za makazi katika kijiji cha Mwanzega wilayani Mkuranga ambako Mwenge wa Uhuru ulifika na kuweka jiwe la msingi Julai 22, mwaka huu.
zaidi ya miaka 5 iliyopita
UZINDUZI wa albamu ya Kamata Pindo la Yesu ya Rose Muhando baada ya jijini Dar es Salaam inatarajia kuendelea katika mikoa ya Tabora na Geita.
CHAMA cha Darts Tanzania (TADA) kimesema klabu bora itakayofanya vizuri kwenye michuano ya kutafuta klabu bingwa mwezi ujao itashiriki michuano ya wazi ya Uganda itakayofanyika Septemba nchini Uganda.
BEKI wa zamani wa Yanga, Omary Kapilima ni mgombea pekee wa nafasi ya uenyekiti wa klabu ya soka ya daraja la tatu ya Scud ya Mtoni Mtongani, Dar es Salaam.
NAHODHA wa Tanzania katika Michezo ya 20 ya Jumuiya ya Madola, bondia Selemani Kidunda amepigwa katika pambano lake la juzi usiku dhidi ya Kehinde Ademuyiwa wa Nigeria jijini Glasgow, Scotland.
KLABU ya Yanga imesema haijajitoa kushiriki kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuwania Kombe la Kagame isipokuwa wanasubiri kupewa ratiba.
MSANII wa muziki wa Injili, Bahati Bukuku (40), ni miongoni mwa majeruhi watatu wa ajali ya gari iliyotokea ilitokea katika barabara ya Morogoro – Dodoma eneo la Ranchi ya Narco Wilaya ya Kongwa.
MSHAMBULIAJI wa Mtibwa Sugar ya Morogoro, Juma Luizio amefuzu majaribio katika timu ya Zesco United ya Zambia alikokwenda mapema wiki hii kujaribu bahati yake.
MWENYEKITI wa Klabu ya Yanga, Yusuf Manji na Makamu wake, Clement Sanga wametangaza kuvunja kamati zote ambazo ziko chini ya Kamati ya Utendaji kuanzia Alhamisi wiki hii na kuteua kamati nyingine yenye wajumbe 10 watakaosimamia masuala mbalimbali yanayohusu Yanga.
TANZANIA bado haijafanya vizuri katika Michezo ya 20 ya Jumuiya ya Madola inayoendelea jijini Glasgow, Scotland, baada ya wanariadha kushindwa katika mbio za marathoni jana na katika ndondi, bondia mmoja tu amefanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali.