NAMBIE mdau mambo vipi, wanasemaje waungwana hapo, mambo yanaenda au kila kukicha afadhali ya jana? Namshukuru Mungu kwa yote, sitachoka kuomba baraka zake sanjari na msamaha ninapotenda kinyume na anavyotaka yeye. Nimezungumzia msamaha kwa kuwa naamini si tu ni muhimu katika uhusiano wangu na yeye lakini pia, katika uhusiano wangu na wanadamu wengine.