WAKATI Promosheni ya Timka na Bodaboda inayoendeshwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania ikielekea ukingoni, neema imeendelea kuwashukia maelfu ya Watanzania na safari hii, Wilson Urio, fundi viyoyozi mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar es Salaam amejishindia Sh milioni 20.
zaidi ya miaka 7 iliyopita
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo imekabidhi zawadi za fedha Sh milioni 160 kwa washindi 375 wa promosheni ya ‘Cheza Unaposhinda Kitita na Tigo Pesa’ katika hafla iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
UONGOZI wa Mkoa wa Kagera umeiomba Serikali kuliomba Shirika la Ndege nchini (ATCL) kuanzisha safari za ndege kutoka Dar es Salaam hadi Bukoba ili kuongeza ushindani wa kibiashara na makampuni mengine na hivyo kusaidia kupunguza mzigo wa nauli wanaobebeshwa wakazi wa mkoa huo.
MATUMBAWE bandia yaliyowekwa katika eneo la ghuba ya pwani ya Chwana na Marumbi, yameanza kuingiza samaki wa aina mbali mbali na kuleta matumaini mapya kwa wavuvi kuongeza kipato.
WANANCHI wa Wilaya ya Uyui mkoani Tabora wameomba Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati kupanda kwa bei ya umeme na gesi .
KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel Tanzania imewazawadia wateja wake zaidi ya Sh milioni 130 na kutoa tiketi 12 za safari iliyolipiwa kila kitu kwenda Old Trafford, Uingereza kupitia promosheni yake ya ‘Mimi ni Bingwa’.
KAMPUNI ya Mawasiliano Tanzania (TTCL) imewashawishi Watanzania kuendelea kutumia huduma zake huku ikiahidi mwaka huu kuimarisha huduma zake katika sauti, data na intaneti.
KAMPUNI ya simu za mkononi imetoa Sh milioni 160 kwa wateja wake katika droo ya pili, iliyochezeshwa katika promosheni yake ya ‘Shinda Kitita na Tigo Pesa’.
SERIKALI imewaagiza wafanyabiashara kuanzia leo kila mfanyabiashara kununua Mashine za Kielektroniki za (EFDs) za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
WAFANYABIASHARA jijini hapa jana walifunga maduka yao, kupinga kutumia mashine za kielektroniki (EFD) za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), zinazotumika kutoa risiti wakati wa kuuza bidhaa zao.