Takukuru yabaini mapungufu miradi yenye thamani ya Sh Bil 5

TANGA; Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Tanga imebaini mapungufu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh bilioni tano.

Akiongea na waandishi wa habari Ofisa uchunguzi mwandamizi katika taasisi hiyo Mkoa wa Tanga Frank Mapunda wakati wa kutoa taarifa ya utendajikazi wa taasisi hiyo katika kipindi cha kuanzia mwezi Julai hadi Septemba mwaka huu.

Amesema kuwa mapungufu hayo wameyabaini baada ya kufanya ukaguzi kwenye miradi 60 yenye thamani ya Sh bilioni 10.6 ambapo miradi 28 ndio ilibainika kuwa na mapungufu mbalimbali ikiwemo ununuzi wa vifaa vilivyochini ya kiwango na ujenzi usiozingatia maelekezo ya ramani.

Aidha katika kutekeleza jukumu la uzuiaji wa Rushwa taasisi hiyo mkoani Tanga imefanikiwa kufanya uchambuzi wa mifumo tisa Ili kupata mifumo imara isiyokwamisha utoaji wa huduma bora Kwa wananchi na utendajikazi za serikali.

Vile vile Mapunda amesema katika utekelezaji wa Programu ya TAKUKURU rafiki wameweza kutembelea kata 22 na kupokea kero zaidi ya 390 za vitendo vya rushwa huku kero 107 zikiweza kupatiwa ufumbuzi.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Angila
Angila
18 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online. Get this today by follow instructions……
.
.
.
On This Website……………..> > W­w­w.S­m­a­r­t­c­a­r­e­e­r­1.c­o­m

Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x