Tamasha la ZIFF lapata Mkurugenzi mpya

MUONGOZAJI wa filamu nchini Amil Shivji ameushukuru uongozi wa tamasha la Kimataifa la Filamu la Nchu za Jahazi Zanzibar (ZIFF) kwa kumchagua na kumtangaza kuwa mkurugenzi mpya watamasha hilo.

Shivji akipokea kijiti toka kwa mkurugenzi wa awali Profesa Martin Mhando amesema tamasha hilo lenye miaka zaidi ya 26 limemuheshimisha yeye kampuni za filamu nchini pamoja na waigizaji wote nchini.

Awali akizungumza wakati wa kukabidhi nafasi hiyo aliyodumu nayo kwa zaidi ya miaka 15, Prof. Martin Mhando amemuelezea, Shivji kuwa ni chachu inayohitajika katika uongozi wa Tamasha hilo kutokana na weredi wake katika sanaa.

Shivji ameshatayarisha filamu kadhaa na zimeshinda tuzo mbalimbali za kitaifa na kimataifa filamu hizo ni pamoja na ‘Vuta N’kuvute’ (2022) na ‘T-Junction’ (2017).

Shivji ni msomi aliyefuzu Chuo Kikuu cha York na mwenye Shahada ya Uzamili ya Sanaa katika Utayarishaji wa Filamu kutoka Toronto, Canada,
lakini pia, ndiye mwanzilishi wa Kijiweni Productions, taasisi ya utayarishaji filamu.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Julia
Julia
1 month ago

Earn money in USA, high scores from trusted resources. Work at your own pace. Regular Payments. Search in different job categories. Work anywhere on your vs03 computer, laptop or mobile phone. Update your profile at any time.
.
.
Detail Here———->>> http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Julia
Angelhompson
Angelhompson
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Angelhompson
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x