Tanzania, Afrika Kusini za saini hati ya makubalino

Ni ya kuboresha sekta ya afya

SERIKALI  kupitia Wizara ya Afya imeingia makubaliano na  Afrika Kusini  ya ushirikiano katika sekta ya afya ili  kuboresha zaidi huduma za afya na ushirikiano wa pamoja katika kubadilishana uzoefu na watalaam katika sekta hiyo.

Makubaliano hayo yamefanyika kati ya Waziri wa Afya,  Ummy Mwalimu na Waziri wa Afya Afrika Kusini Dkt. Mathume Joseph Phaahla Jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

Viongozi hao wamekubaliana kuwa na mpango wa utekelezaji na ufuatiliaji wa mkataba huo na kutoa taarifa kila mwaka.

“Tanzania na Afrika Kusini zimekuwa na ushirikiano wa muda katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya Afya, kusainiwa kwa hati hii kutachangia  kuboresha ushirikiano katika sekta ya afya.”Amesema Ummy

Akifafanua  Ummy amesema, nchi hizo mbili zitabadilisha  wataalam wabobezi kwenye fani mbalimbali za afya, kuwezesha mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu na kubadilishana teknolojia, kuboresha upatikanaji wa dawa, chanjo na udhibiti wa magonjwa ya mlipuko pamoja na dharura za Afya.

Amesema, ushirikiano kati ya nchi hizo mbili utaimarisha mfumo wa huduma za  rufaa kwa wagonjwa watakaohitaji matibabu nchini Afrika Kusini.

Aidha, amesema ksainiwa kwa hati hiyo ni moja ya maazimio ya Mkutano wa Pili wa mataifa mawili (Bi – National Commission – BNC)  baina ya  Tanzania na Afrika kusini ambapo  Azimio namba  43 lilielekeza kwamba,  hati  ya makubaliano katika sekta ya afya isainiwe  baada ya taratibu zote ambapo Rais  Samia Suluhu Hassan,  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais  Cyril Ramaphosa wa Jamhuri ya Afrika Kusini walisisitiza umuhimu wa kutekeleza maafikiano yaliyofikiwa na kutoa mrejesho wa utekelezaji kwa wakati.

Nae, Waziri wa Afya ya Afrika Kusini, Dkt. Phaahla, amepongeza hatua ya kusainiwa kwa hati ya makubaliano hayo ambayo imefanyika katika kipindi ambacho  dunia nzima inakabiliwa na majanga mbalimbali ya mlipuko ikiwemo mabadiliko ya tabia nchi.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button