Tanzania kuanzisha minada ya madini

WAZIRI wa Madini, Dk Doto Biteko amesema wanatarajia kuanzisha minada ya madini kwa lengo la kupata wanunuzi wakubwa wa kimataifa ili waje kununua madini hayo kwa bei kubwa zaidi kuliko ilivyo sasa.

Dk Biteko aliyasema hayo jana Mirerani, Simanjiro mkoani Manyara wakati akikagua maendeleo ya Kitalu C na ujenzi wa Tanzanite Centre.

“Rais amekubali tuanzishe utaratibu wa kutafuta wanunuzi wakubwa wa madini waje ili mawe kidogo mnayopata yapate thamani kubwa kuliko ilivyo sasa na tumepata mwekezaji mpya anaitwa Franone ambapo kwa kipindi cha miezi sita amezalisha ajira 328,” alisema.

Alisema utaratibu wa kufanya biashara ya madini ndani ya ukuta ni biashara huru na kuwataka wafanyabiashara wa madini ndani ya ukuta kuuza mawe yao kwa mtu wanayemtaka bila kusumbuliwa lakini pia jiwe linalotoka ndani ya ukuta lazima lihesabiwe na kujulikana thamani yake na sehemu linapokwenda.

Naye Mbunge wa Jimbo la Simanjiro, Christopha Ole Sendeka, alimpongeza Dk Biteko kwa kuleta utulivu kwenye sekta ya madini na kumuomba aendelee kuwa balozi katika kuendeleza utulivu kwenye sekta hiyo.

Kwa upande wake, Ofisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Kimadini Mirerani, Bernard Msengi alisema kwa mwaka wa fedha 2022/23 ofisi yake imekusanya kiasi cha Sh bilioni 2.6 sawa na asilimia 52.23 ya lengo la makusanyo huku akieleza sababu zilizosababisha baadhi ya malengo kutofikiwa ni pamoja na hali ya kijiolojia ya mashapo kuwa katika kina kirefu hivyo migodi mingi kutumia muda mrefu kufanya utanuzi na uwekezaji wa migodi pamoja na ukosefu wa teknolojia za kisasa kwa wachimbaji wadogo ndani ya eneo la ukuta.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Drinnera1939
Drinnera1939
2 months ago

Im making over $23k a month working part time. I kept hearing other people tell me how much money they can make online so I decided to look into it. Well, it was all true and has totally changed my life. This is what I do.========>=====>>>http://www.dailypro7.com

Kathleen D. Holloway
Kathleen D. Holloway
Reply to  Drinnera1939
2 months ago

I currently make about 6000-8000 dollars /month for freelancing I do from my home. For those of you who are ready to complete easy online jobs for 2-5 h every day from the comfort of your home and make a solid profit at the same time
.
.
Try this work______  https://fastinccome.blogspot.com/

Zambia Revenue Authority
Zambia Revenue Authority
Reply to  Kathleen D. Holloway
1 month ago

Zambia Revenue Authority

MAPINDUZII.PNG
Zambia Revenue Authority
Zambia Revenue Authority
Reply to  Drinnera1939
1 month ago

Zambia Revenue Authority

MAPINDUZII.PNG
Mining Census 2023
Mining Census 2023
1 month ago

Mining Census 2023

Watanzania mnakaribishwa kwenye SENSA ya Madini 2023 yenye lengo la kujua idadi ya migodi Tanzania, Idadi ya wachimbaji au watanzania wanaoshughulika na sekta ya Madini, Hali ya uchimbaji wa madini (zana zitumikazo kwa kila mgodi) na mapendekezo ya mbinu za kuboresha Sekta ya Madini.

Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x