Tanzania, Malawi kushirikiana kuzalisha umeme

TANZANIA na Malawi zimeingia makubaliano ya ushirikiano katika nishati, ikiwa kutekeleza agizo la wakuu wa nchi hizo mbili.
Akizungumza leo Agosti 11, 2023, Waziri wa Nishati January Makamba, amesema wameingia makubaliano hayo, ili kuimarisha sekta ya nishati katika nchi zote mbili na kuweka bayana makubaliano hayo.
“Makubaliano yetu katika sekta ya nishati yanahusu maeneo matatu, kwanza kabisa kuzalisha umeme kwa pamoja kwenye mradi wa kuzalisha umeme kwa nguvu ya maji katika mto Songwe.
“Ushirikiano katika utafutaji, utafiti na uchimbaji wa pamoja wa gesi na mafuta na kushirikiana katika ujenzi wa miundombinu ya umeme, “ amesema Waziri Makamba.
Makamba amesema makubaliano baina ya serikali hizo mbili yapo katika utaratibu maalumu, ambapo kutakuwa na kamati ya pamoja ya mawaziri na kamati ya wataalamu ya kufuatilia utekelezaji wa makubaliano hayo, ambapo kila nchi itateua wataalamu ndani ya mwezi mmoj,a huku vikao rasmi vinatarajiwa Oktoba mwaka huu.
Kwa upande wake Waziri wa Nishati wa Malawi, Ibrahim Matola amesema makubaliano hayo ni utekelezaji wa maagizo ya wakuu wa nchi hizo mara baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kufanya ziara nchini Malawi, lakini pia ziara ya Rais wa Malawi Lazarus Chakwera kutembelea Tanzania.
Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet…
Check The Details HERE….. https://webonline76.blogspot.com/
Ratiba ya Ziara ya Mary Pius Chatanda KIONGOZI wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) KWENYE SEKTA YA MADINI ATATEMBELEA:-
· Mgodi wa Dhahabu
· Mgodi wa Almas
· Mgodi wa Gas
· Mgodi wa Uranium
· Mgodi wa Mafuta
· Mgodi wa Makaa ya mawe
· Mgodi wa Tanzanite
Kuanzia tarehe 23/8/2023 hadi tarehe 2/8/2023