Tanzania, Qatar zakubaliana vyeti vya mabaharia

LONDON; Serikali ya Tanzania na Serikali ya Qatar zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya kutambuliana vyeti vya mabaharia katika hafla ya utiaji saini iliyofanyika jijini London.
Hafla hiyo imefanyika pembezoni mwa mkutano wa 34 wa Baraza Kuu la Shirika la Bahari Duniani na kuhudhuriwa na viongozi pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya bahari.
Kwa upande wa Tanzania, makubaliano hayo yamesainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mohamed Malick Salum, huku Mhandisi Abdulaziz Abdullah Al-Sulait, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi wa Qatar, akisaini kwa niaba ya nchi yake.
Kupitia MoU hiyo, pande zote mbili zinatarajia kuboresha viwango vya umahiri, usalama na ubora katika taaluma ya ubaharia, sambamba na kuendeleza uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na Qatar.

Hatua hiyo inatarajiwa kuongeza ajira kwa mabaharia wa Kitanzania katika meli zilizosajiliwa au kuendeshwa na kampuni za Qatar, kwani hawatalazimika kupitia upya taratibu za uthibitishaji wa vyeti pamoja na kuimarisha ushirikiano katika sekta ya usafirishaji baharini kati ya nchi hizo mbili.
Aidha makubaliano haya yatawezesha mabaharia kupata maslahi bora na fursa zaidi za kazi kwenye masoko yenye ushindani wa juu na kunachochea uhamishaji wa ujuzi na utaalamu wa kimataifa.
Hatua hiyo itasaidia kwa kuwa mabaharia watafanya kazi katika majukwaa yenye viwango vya juu vya teknolojia na usalama pamoja na kuimarisha uwezo wa Tanzania katika utoaji wa mafunzo ya ubaharia, kwani vyuo na vyeti vyake vitakuwa na uhalali mpana zaidi kimataifa.-



JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Google provides awesome remote work opportunities, allowing me to earn $2000-$3000 weekly with just 2-4 hours of daily work. It’s been a game-changer, offering flexibility and reliable income. If you’re seeking a genuine way to earn online, don’t miss this chance. Start today and transform your life!
.
More Details For Us →→ http://www.big.income9.com