TAWA kuimarisha ulinzi wa wananchi dhidi ya wanyamapori

MOROGORO:Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), imesema itaendelea kuimarisha  ulinzi wa wananchi na mali zao dhidi ya wanyamapori wakali na waharibifu.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Uhifadhi  Dar es Salaam  wa Mamlaka  hiyo , Kamishna Msaidizi Mwandamizi , Sylvester Mushi amesema hayo  wakati akimkaribisha Mkuu wa wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro, Judith  Nguli.

Advertisement

Mkuu huyo wa wilaya alikuwa mgeni rasmi wa  kuzindua  vikundi  12 vya kujitolea vya kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu , na ugawaji  vifaa  vilivyotolewa  Mamlaka hiyo.

Hafla hiyo imefanyika kwenye   Kata ya Melela, Tarafa ya Mlali wilayani humo ambapo  vikundi  hivyo vya kujitolea kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu vimeundwa kutoka vijiji 11 vilivyopo katika kata nne  za Wilaya Mvomero zenye changamoto kubwa ya Wanyamapori wakali na Waharibifu.

Kata hizo zipo kwenye eneo linalosimamiwa na Mamlaka hiyo ambazo ni Melela, Lubungo, Mlali na Dakawa (Wami Dakawa), ambapo  vikundi hivyo vilivyopatiwa  mafunzo vimegawiwa   vifaa ambavyo ni tochi  za mwanga mkali 120, vuvuzela 120 na filimbi, 120 thunder flash 600 na roman candle 600 na vitakuwa na uwezo wa kudhibiti wanyamapori watakaovamia mashamba na  mazao kwa haraka kabla askari wahifadhi kufika.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Uhifadhi  inajumuisha mkoa wa Pwani, Dar es Salaam na Morogoro  amesema hatua hiyo  ni  kupunguza madhara yanayosababishwa  wanyamapori hususani tembo kwenye uharibifu wa mazao ya wananchi.

 

 

5 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *