Timu nne kundi la Stars zafungana pointi

MSIMAMO wa kundi E lenye timu sita, timu nne zina pointi 3 ikiwemo Tanzania, licha ya kuwa mbele kwa mchezo mmoja dhidi ya Morocco na DR Congo ambao hawana alama yoyote.
–
Baada ya kupoteza leo mabao 2-0 dhidi ya Morocco, Tanzania imeshuka hadi nafasi ya nne katika msimamo wa kundi hilo lenye timu za Zambia, Morroco, Eritrea, DR Congo, na Niger.
–
Niger na Zambia wana pointi sawa na Tanzania 3 na wote wameshacheza michezo miwili.
–
Eritrea hawashiriki kwa sababu walishajiondoa kwenye kushiriki kufuzu Kombe la Dunia.