Toeni tafiti kusaidia jamii – Isaka

VIJANA  wanaofanya tafiti katika nyanja mbalimbali katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)wameagizwa kutoa matokeo ya tafiti zao  ili kutatua  changamoto zinazoikabili jamii.

Rai hiyo imetolewa leo na Dk,Irene Isaka  ambaye ni Mkurugenzi wa Sekta za Jamii Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika kongamano  linalohusu  Maendeleo ya Teknolojia kupitia tafiti mbalimbali lililoandaliwa na Taasisi ya Afrika ya  Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) kwa kushirikiana na  GIZ .

Advertisement

Amesema  kuwa  endapo watafiti vijana wakitoa matokeo ya tafiti zao kwa jamii serikali za nchi za EAC kila moja zinaweza  kuchukua hatua za mabadiliko ya tabia nchi .

“Lazima sasa wasomi vijana wanapofanya tafiti zao wazitoe zisomwe ili serikali na jamii zichukue hatua katika kukabiliana na changamoto zilizoibuliwa”

Naye Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela ,Profesa Emmanuel Luoga amesema kuwa CENIT@EA ni kituo cha Umahiri kinachojihuisha na masuala ya  Kompyuta na Tehama kinahusisha nchi zote za Afrika Mashariki kwa lengo la kuhakikisha masuala ya tafiti yanaibuliwa ili kutoa majibu sahihi ya changamoto za jamii na kuibua ajira.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *