DAR ES SALAAM: RAIS Samia Suluhu Hassan amesema katika kukabiliana na rushwa nchini, trafiki barabarani wanapaswa kuondolewa badala yake taa na kamera zitatumika kuongoza barabarani.
Rais Samia ameyasema hayo leo, Ikulu jijini Dar es Salaam katika hafla ya kuapisha viongozi wateule wa ngazi mbalimbali za uongozi nchini.
“Usalama barabarani, tunataka kuondoa trafiki barabarani kukomesha rushwa. Tuyaache mambo ya pita wewe nenda wewe,” amesema Dk Samia