Trump atangaza nia kurudi Ikulu Washington

Rais wa Zamani wa Marekani, Donald Trump

RAIS wa zamani wa Marekani, Donald Trump ametangaza kuwania tena kiti cha urais wa nchi hiyo ifikapo 2024 licha ya kukabiliwa na uchunguzi wa uhalifu na utendakazi mbaya.

“Ili kuifanya Marekani kuwa kubwa tena, usiku wa leo natangaza nia yangu ya kuwania Urais wa Marekani,” Trump , mwenye miaka 76, aliuambia umati wa watu na wafuasi wake. Ninagombea kwa sababu ninaamini ulimwengu bado haujaona utukufu wa kweli wa taifa hili.

Kuna safari ndefu kabla ya mgombea mteule wa urais wa chama cha Republican kuchaguliwa rasmi katika majira ya kiangazi ya Marekani 2024, huku kukiwa na mchujo wa kwanza wa ngazi ya serikali ukiwa umebakiza zaidi ya mwaka mmoja.

Advertisement

Wachambuzi wanaamini kuwa uzinduzi wa mapema usio wa kawaida wa Trump unaweza kuwa na lengo la kuwaepusha wapinzani wanaoweza kuwania uteuzi wa chama hicho mnamo 2024, akiwemo Gavana wa Florida anayeinukia Ron DeSantis, 44, na makamu wa rais wa zamani wa Trump, Mike Pence, 63.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *