MTWARA; MKURUNGEZI Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), Tuma Abdallah amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Ahmed Abbas kuhusu namna bora ya kuboresha uhusiano na ushirikiano baina ya kampuni hiyo na mkoa.
Mazungumzo hayo yamefanyika leo Novemba 16 ,2023 katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huyo mjini Mtwara, ambapo pia Mkurugenzi Mtendaji huyo ametembelea na kufanya mazungumzo na baadhi ya wadau na wakuu wa taasisi za serikali mkoani humu.
Pamoja na mambo mengine, wakuu hao walijadili pia namna ya kuboresha mazingira ya kibiashara na uwekazaji.
Tuma aliambatana na Kaimu Mkurungezi wa Maendeleo ya Biashara Felix Mushi, Kaimu Meneja wa Huduma za Kiswahili Mgaya Kingoba na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano kwa Umma Oscar Mbuza.