TTB, Njombe waipangia mikakati hifadhi ya Kitulo

BODI ya Utalii nchini (TTB), imepanga kuinua utalii uliopo  Nyanda za Juu  Kusini, husuani mkoa wa Njombe katika hifadhi  ya Kitulo, ikiwa ni kuendeleza program ya  kukuza utalii nchini kupitia  ya filamu ya Royal Tour.

Hifadhi hiyo ina aina mbalimbali za maua zaidi ya 200, lakini pia ikiwa na utalii mkubwa wa ndege kuhama kutoka Njombe kwenda Ulaya na kurejea tena.

Kaimu Mkurugenzi wa TTB, FeliX John, amesema hayo leo Dar es Salaam, wakati akielezea uzinduzi  mkakati na  maonesho ya vivutio vya utalii vya eneo hilo, yatakayoanza kesho Septemba 25 na kilele chake kuwa Septemba 27, ambayo ni  siku ya utalii duniani.

Amesema wajibu wa Bodi  hiyo ni pamoja na kuongeza vivutio vya utalii nchini, ikiwa ni  sehemu ya utekelezaji wa filamu ya Royal Tour, kukiwa na lengo la kufikia idadi ya watalii milioni tano, kufikia mwaka 2025.

Kuhusu maonesho ya utalii Njombe, Mkuu wa mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amesema kupitia maonesho hayo wanaiambia dunia kuwa hifadhi ya Kitulo  ni maalum na ya kipekee, ikisheheni maua ya aina mbalimbali.

Amewataka wawekezaji kuwekeza katika eneo hilo, hususani katika eneo la hoteli na kwamba ardhi ipo ya kutosha na yenye kuhimili hali ya hewa iliyo nzuri kwa kipindi chote.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button