‘Tutaendelea kushirikiana ili kukuza uchumi’

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), itaendeleza na kuimarisha ushirikiano  na serikali ya Muungano wa Tanzania  katika nyanja mbalimbali, zikiwemo sekta ya kilimo, utalii, na biashara, ili kukuza uchumi wa pande zote mbili za muungano.

Hayo yamesemwa  Waziri wa Klimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo  wa  SMZ , Shamata  Shaame Khamis  mjini Morogoro,  wakati  wa ziara ya Kamati ya Bunge inayosimamia Kilimo, Biashara na Utalii kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar.

Kamati hiyo ilikutana na kufanya mazungumza na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Fatma Mwassa pamoja na sekreterieti ya mkoa huo na kutembelea Kituo  cha Utafiti cha Kilimo (TARI) Dakawa,wilayani Mvomero kwa ajili ya kujifunza mambo mbalimbali hususani kilimo cha mpunga.

Khamis amesema  wizara yake imeweka mkakati maalumu kwa kuhusisha watendaji wa pande zote mbili za Muungano kutoka  wizara hizo  kwa mujibu  wa  maelezo ya viongozi wakuu  walioelekeza  kuwa na ushirikiano na vikao kati ya wizara na taasisi nyingine .

pharmacy

“Viongozi wetu wanatupa ushirikiano na hata tulipoomba  ruhusa ya kuja huku  (Morogoro), viongozi wetu waliridhia  maana yake ni kwamba  wanataka mabadiliko na mabadiliko hayo ni kwenye uzalishaji  kwenye sekta zetu za kilimo za pande zote mbili,” amesema.Naye Mkuu wa Mkoa ,Fatma Mwassa, ameipongeza  kamati hiyo kutembelea Mkoa wa Morogoro, ili kujifunza mambo mbalimbali hususani kilimo cha zao la mpunga.

Amesema  kuwa  zao la mpunga  ndiyo zao kubwa la kimkakati na Tanzania kwa ujumla, kwani mkoa kwa sasa unashika nafasi ya kwanza kwenye  uzalishaji wa mpunga  nchini.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button