Twendeni tukaujaze!

DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro amewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani kushuhudia michezo miwili ya michuano mipya ya African Football League (AFL), itakayochezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Dk Ndumbaro amesema ni heshima kwa nchi kuaminiwa na kuteuliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa michuano ya AFL kuzinduliwa kwa mara ya kwanza katika ardhi ya Tanzania, ambapo Simba SC ya Dar es Salaam itavaana na Al Ahly ya Misri.

Aidha, kiongozi huyo amesema Tanzania imepewa nafasi ya kuwa mwenyeji wa mchezo wa pili AFL kutokana na wakaguzi wa CAF kuvutiwa na utendaji unaofanyika nchini sambamba na huduma bora zinazotolewa ikijumuisha maeneo bora ya viwanja vya michezo, huduma bora za hoteli, usafirishaji salama wa abiria na mizigo.

“Mechi kati ya TP Mazembe DRC dhidi ya Esperance ya Tunisia iliyopaswa kuchezwa pale Lubumbaji, imehamishiwa Dar es Salaam, tumepewa sisi Tanzania na utapigwa Uwanja Benjamin Mkapa, na utachezwa Oktoba 22, 2023,” amesema Dk Ndumbaro.

Amesema ujio wa AFL nchini ni fursa kwa sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya utalii, sekta ya michezo, sekta ya biashara na uimarishaji wa masuala ya kijamii na kidiplomasia.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Mpango wa Kujitathmini Kiutawala Bora Barani Afrik
Mpango wa Kujitathmini Kiutawala Bora Barani Afrik
1 month ago

Mpango wa Kujitathmini Kiutawala Bora Barani Afrika (APRM)

Work AT Home
Work AT Home

I’ve earned $17,910 this month by working online from home. I work only six hours a day despite being a full-time college student. Everyone is capable of carrying out this work from their homes and learning it in spare time on a continuous basis.

To learn more, see this article———>>> http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x