Uhuru Kenyatta ataka waasi DRC kuweka silaha chini

MAPIGANO kati ya vikosi vya serikali na waasi wa M23 yanaendelea Mashariki mwa DRC karibu na mji wa kimkakati wa Goma katika jimbo la Kivu Kaskazini na Rais wa zamani wa Kenya ambaye ni mpatanishi wa EAC Uhuru Kenyatta amewasili Kinshasa kwa mazungumzo ya amani ambayo yatafanyika Novemba 21.
“Ujumbe tulionao leo ni kwamba makundi yote yanayobeba silaha kwa sasa yaweke chini silaha hizo na kuchagua njia ya amani kwa njia ya mazungumzo kwa sababu hakuna kitu kinachoweza kupatikana kupitia mtutu wa bunduki”, alisema Uhuru Kenyatta, Rais wa zamani. wa Kenya na mwezeshaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu Mchakato wa Amani katika eneo la Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Serikali ya Kongo inaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi, tuhuma ziliyokataliwa na Kigali.
“Weka chini bunduki na ujiunge katika mchakato wa kisiasa. Hiyo ni kwa makundi ya ndani. Kwa makundi ya kigeni, kimsingi inasema kwamba DRC sio tena uwanja wa vita kwa matatizo ambayo hayatoki katika nchi hii”, aliongeza Rais huyo wa zamani.
Mashariki mwa DRC ilikuwa ukumbi wa vita viwili vya umwagaji damu katika miaka ya 1990 na kuacha makundi mengi yenye silaha ambayo yamesalia hai katika eneo hilo.