Urusi yadai Vatican imeiomba radhi kufuatia kauli ya Papa

VATICAN imeomba msamaha kwa Urusi baada ya Papa kudai makabila mawili yanayopigana katika operesheni ya kijeshi ya Urusi nchini Ukraine yalikuwa na “ukatili zaidi”.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imesema Vatican imeomba msamaha kwa kauli ya Papa Francis aliyoitoa hivi karibuni katika mahojiano ambapo alitaja makabila mawili madogo ya Kirusi – Wachechnya na WaBuryats – kuwa washiriki “wakikatili zaidi” katika vita vya Ukraine.
Katika kikao kifupi, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi, Maria Zakharova, alinukuu kutoka kwa kile alichosema kuwa ni ujumbe kutoka Vatican kwamba “unaomba msamaha kwa upande wa Urusi” kwa maoni ya Papa.
Zakharova, alisifu ujumbe huo, akisema kwamba unaonesha “uwezo wa Vatican wa kufanya mazungumzo na kusikiliza.”
Msemaji wa Vatican alisema kumekuwa na mawasiliano ya kidiplomasia kuhusu suala hilo.
Papa huyo mwenye umri wa miaka 85 alitoa maoni kuhusu Wachechnya na Waburuya wakati wa mahojiano na jarida la Jesuit la Marekani mwezi uliopita.
“Wakatili zaidi labda ni wale ambao ni wa Urusi lakini sio wa mila ya Kirusi, kama vile Wachechnya, WaBuryats na kadhalika,” aliambia chombo hicho. “Nazungumza juu ya watu waliouawa kishahidi. Ikiwa una watu waliouawa kishahidi, wapo wahusika.”
Francis amezungumza mara kwa mara kuhusu watu “waliouawa” wa Ukraine tangu Urusi ilipovamia Februari 24.
The point of view of your article has taught me a lot, and I already know how to improve the paper on gate.oi, thank you. https://www.gate.io/pt/signup/XwNAU