Ushetu wajipanga ukarabati wa barabara

HALMASHAURi ya  Ushetu  wilayani Kahama mkoani Shinyanga,  imetenga jumla ya Sh Millioni 20 katika bajeti ya mwaka 2022/2023  kwa ajili ya ukarabati wa barabara.

Hayo yamesemwa leo kwenye kikao cha  kawaida cha Baraza la  Madiwani, wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi, Uchumi na Mazingira,   ambaye ni diwani wa kata ya Bukomela, Kulwa Shoto akiwasilisha taarifa  juu ya kamati hiyo.

Amesema kuwa  greda lilifanya kazi na kuharibika baada ya kutengeneza kilomita 21 na kwamba bado liko kwa fundi..

Diwani  Viti Maalum,  Ester Matone amesema  kwa taarifa waliyonayo wameelezwa mtambo umeingiza kiasi cha Sh milioni 18.7,  lakini matengenezo ya greda yametumia Sh milioni  4.5, hivyo  wametaka greda hilo liwanufaishe sababu barabara wanaziona bado changamoto ya kutopitika.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo,  Linno Mwageni amesema kulikuw na changamoto ya uaminifu kwa dereva aliyekuwepo, hivyo wamepata dereva mwingine anaamini mambo yatakuwa mazuri.

 

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button