Usitishaji vita Israel, Hamas bado kitendawili

USITISHAJI vita wa muda kati ya Israel na Hamas umeingia siku ya tano na sasa zimeongezwa saa 48 kukubaliwa kwa mkataba huo.

Taarifa ya BBC imeeleza kuwa Wapalestina watatu wataachiliwa kutoka magereza ya Israel.

Kundi la jeshi la Hamas limesema haliwashikilii mateka wote katika Ukanda wa Gaza, na kwamba kufanya hivyo kunaweza kukwamisha kuwakomboa walio hatarini zaidi.

Mashambulizi ya Hamas ya Oktoba 7, yaliuwa takribani watu 1,200 na 240 kuchukuliwa mateka tangu wakati huo.

Wakati huohuo, Wizara ya Afya Gaza inayoendeshwa na Hamas imesema zaidi ya 14,500 wameuawa katika kampen ya Israel kulipiza kisasi.

4 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *