Utafiti: Watanzania wanajenga nyumba kwa miaka18

*Asilimia 70 wanapanga

DAR ES SALAAM: Asilimia 70 ya watanzania wanaishi katika nyumba za kupanga huku wanaojenga wakichukua muda mrefu zaidi ya miaka 18.

Hayo yameelezwa katika ripoti ya utafiti wa ‘Housing Microfinance (HMF)’
uliofanywa na Shirika la Habitat for Humanity International (HFHI) na Tanzania Mortgage Refinance Company (TMRC) iliyozinduliwa Novemba 9, 2023 jijini Dar es Salaam.

Utafiti huo ulifanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Dodoma kwa wananchi wenye umri wa miaka 25 hadi 50 wakiangazia hali ya vipato vyao.

Mkurugenzi wa Nyumba na Fedha kutoka Habitat For Humanity Internation, Daniel Mhina akizungumza amesema watanzania wengi hawana kipato cha kumudu kujenga nyumba na wanaojenga huchukua muda mrefu.

“Unapojenga nyumba muda mrefu kwa miaka 18 gharama zinaongezeka, zinakuwa kubwa kuna kurekebisha mabati, kupaka rangi kwa mtanzania wa kawaida anatakiwa kupata mkopo kwenye huduma za kifedha, changamoto tuliyoiona, huduma za kifedha hazina mikopo inayoendana na matakwa ya watanzania,”amesema Mhina

Utafiti huo umeonyesha kuwa kaya nyingi za kitanzania zinaishi kwa kipato cha chini na cha kati zinazopata kati ya Sh 80,000 ($34) hadi Sh milioni 1.5 ($630) kwa mwezi.

Ripoti hiyo inasema wananchi waliohojiwa walidai kuwa wangependelea kukopa na kila mwezi kurejesha sh 5,000 na wengine walipendekeza rejesho kuwa na ukomo wa sh 80,000.

Hata hivyo ripoti hiyo imeonyesha kuwa changamoto kubwa iliyopo kwa wahitaji wa mikopo ni kutokuwa na uwezo wa kumudu vigezo vinavyohitajika katika taasisi nyingi za kifedha ikiwemo mabenki, unyanyapaa na kutoaminika kwa wajengaji.

Hata hivyo, akizungumzia ripoti hiyo, Mhina anasema uhusiano wa Habitat For Humanity Internatinal na TMRC, wameleta taasisi za kifedha pamoja na kuichambua ripoti hiyo ambayo lengo ni kutoka na majibu ya namna ya kuwakwamua watanzania ili waishi kwenye makazi bora.

“Tutatafuta wadau wawili au watatu ambao tutashirikiana nao ili waweze kutoa mikopo, inawezekana kwenye masoko mengine wenzetu Kenya wameweza, nchi nyingine wameweza lakini Tanzania bado,”amesema na kuongeza

“Tunaweza kuwasaidia watu wakapata makazi bora, kwa mfano tumeweza kutoa mkopo wa sh milioni 190 kwa wananchi 400 ukiangalia kwenye mikopo ya kawaida ya kibenki wanaweza kuwasaidia watu 400 katika nyumba zao za makazi.

“Ni changamoto inayotulazimu kuja na suluhisho kwa wananchi wa kima cha chini na cha kati,”amesema

Amesema kima cha chini cha mikopo hiyo ni sh 100,00 hadi sh milioni 2 ambazo mtu ataweza kukopa kwa ajili ya kufanya marekebisho madogo madogo kwenye nyumba yake na kurudisha ndani ya miezi sita.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa TMRC, Oscar Mgaya amesema waliona ipo haja ya kuanzisha mikopo ya nyumba ndogo kwa watu wa kipato cha chini na cha kati ambao wana tabia ya kujenga nyumba zao hatua kwa hatua kwa kutegemea pesa kidogo wanayopata.
“Mikopo hii itawezesha kuchukua mikopo midogo midogo kwa ajili ya kujenga nyumba zao kwa awamu. Kwa mfano, mtu anaweza kuchukua mkopo kujenga msingi, kisha baada ya kurejesha anaweza kuchukua mkopo mwingine kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huo,” amesema.

Kwa upande wa Mwakilishi wa Habitat Tanzania, Fotunata Temu amesema watanzania wemeongezeka kwa mujibu wa sensa ni zaidi ya milioni 60 lakini hakuna makazi bora yenye staha.

Amesema kwa mwaka kuna nakisi karibu nyumba 200,000 kila mwaka, uwezo wa watu kujitengenezea makazi bora ni changamoto, gharama ni kubwa na makazi ni moja ya mahitaji ya binadamu, vipato vya watu ni vidogo.

“Tunaona watu wanavyojenga nyumba kidogo kidogo hata ubora wake unakua sio mzuri ila ndio wafanyaje, ndio maana Habitat tunaingia kusaidia ujenzi wa makazi.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
8 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
NAMONGO FC
NAMONGO FC
22 days ago

IKIFIKA WALIOPO HAWATOSHI… WATANZANIA 3 WANATAFUTWA… 1. MKULIMA MKUBWA (TAASISI ZA SERIKALI) 2. MKULIMA WA KATI (MWEKEZAJI MKUBWA SANA) 3. MKULIMA MDOGO (ANAYELIMA NYUMBANI)..

336385342_23852687669090184_4327056666681808736_n-1699524871.7938-300x300.jpeg
AlmaRankin
AlmaRankin
Reply to  NAMONGO FC
22 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website________ http://Www.Careers12.com

Last edited 22 days ago by AlmaRankin
NAMONGO FC
NAMONGO FC
22 days ago

IKIFIKA WALIOPO HAWATOSHI… WATANZANIA 3 WANATAFUTWA… 1. MKULIMA MKUBWA (TAASISI ZA SERIKALI) 2. MKULIMA WA KATI (MWEKEZAJI MKUBWA SANA) 3. MKULIMA MDOGO (ANAYELIMA NYUMBANI).

400691249_864990868631687_149643332150728266_n-1699514610.2614-1699523863.3682-212x300.jpg
NAMONGO FC
NAMONGO FC
22 days ago

IKIFIKA WALIOPO HAWATOSHI… WATANZANIA 3 WANATAFUTWA… 1. MKULIMA MKUBWA (TAASISI ZA SERIKALI) 2. MKULIMA WA KATI (MWEKEZAJI MKUBWA SANA) 3. MKULIMA MDOGO (ANAYELIMA NYUMBANI)…

400652614_122123967464061853_6811123058608430011_n-1699514588.5978-200x300-1699523844.9688.jpg
NAMONGO FC
NAMONGO FC
22 days ago

IKIFIKA WALIOPO HAWATOSHI… WATANZANIA 3 WANATAFUTWA 1. MKULIMA MKUBWA (TAASISI ZA SERIKALI) 2. MKULIMA WA KATI (MWEKEZAJI MKUBWA SANA) 3. MKULIMA MDOGO (ANAYELIMA NYUMBANI)..

396913935_270519422649565_3279129179102033513_n-1699514567.7649-232x300-1699523827.9501.jpg
NAMONGO FC
NAMONGO FC
22 days ago

USALAMA KAZI MHE TUTAFANYA KWA AJILI YA “MLIMA KILIMAJARO” – LAZIMA TUFANYE KITU KWA AJILI YA TANZANIA USALAMA WETU TUKITEMBELE

OSK-1699526502.5327-300x200.jpeg
Angila
Angila
21 days ago

I get paid over $87 per hour working from home with (Qx)2 kids at home. I never thought I’d be able to do it but my best friend earns over 10k a month doing this and she convinced me to try. The potential with this is endless. 
.
.
.
.
Here’s what I’ve been doing…> > > http://remarkableincome09.blogspot.com

Adrian Mbilinyi
Adrian Mbilinyi
20 days ago

Looo ni kweli kuwa watanzania asilimia 70 wanapanga !!!! utafiti huo ni wa mjini au hata vijijini maana inajulikana kwamba zaidi ya asilimia 70 ya watanzania wanaishi vijijini!

Back to top button
8
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x