Veta wabuni mashine ya kukunja vyuma,

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Kampasi ya Moshi, imebuni mashine maalumu ya kukandamiza kwa ajli ya kukata na kukunja vyuma vya kutengenezea bidhaa mbali mbali ikiwemo vijiko, makofuli, komeo za milango na mageti, nati, bawaba za madirisha, umma na bidhaa nyingine za aina hiyo.

Hayo yamebainishwa leo Julai 2,2023 na mwanafunzi wa mwaka wa pili wa chuo hicho, Petro Daudi katika banda la taasisi hiyo kwenye  Maonesho ya Biashara ya 47 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DTIF) yanayoendelea katika Viwanja vya Sabasaba.

Amesema, kumekuwa na uhitaji mkubwa wa mashine  hiyo ambayo inarahisisha uzalishaji wa  bidhaa kwa wingi.

Advertisement

“Mashine hii ni maalum kwa ajili ya kukata, kutoboa, kukunja, kutokana na vifaa vya uzalishaji vyenyewe vilivyofungwa, na imekuwa mkombozi kwa wazalishaji wa bidhaa za chuma.”Amesema

Nae, mwalimu Irene Muro wa chuo hicho anasema VETA imekuwa ikibuni teknolojia mbali mbali kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi ili wakimaliza masomo yao wapate ujuzi wa kujiajiri wenyewe.

“Vijana wanachangamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa ajira hivyo mashine hii imetoa ufumbuzi wa ajira kwa sababu mwanafunzi ataweza kutengeneza mashine yake mwenyewe kama hii na atafanya shughuli zake.”Amesema Muro na kuongeza

“Lakini vile vile malighafi  zinazotengeneza mashine hii zinapatikana hapa hapa nyumbani na hivyo inatoa unafuu  wa gharama kwa wanunuaji.”Amesema

Amesema, mashine hiyo  awali ilikuwa zinaagizwa nje kwa gharama ya sh milioni 13 lakini kwa sasa inapatikana hapa hapa nchini kwa gharama ya sh milioni 3.5

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *