Viongozi wa dini Morogoro wakubali mabadiliko sheria ya ndoa

VIONGOZI wa dini wameungana na serikali katika mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971. Wamesema sheria hiyo inawanyima haki watoto wa kike kutimiza ndoto zao kwa kujikita wakitengeneza familia wakiwa na umri mdogo.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili Kilutheli Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Morogoro, Jacob Mameo Ole Paul, amesema hayo katika maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Kike Duniani iliyoandaliwa na Mradi wa Hapana Marefu yasiyo na Mwisho, unaotekelezwa na C-Sema, Amani Girls kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).

“Sisi viongozi wa dini tuko mstari wa mbele katika mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971,ndoa za utotoni hazikubaliki.” amesema Askofu Mameo.

Askofu Mameo ameishauri serikali kuendelea na mchakato wa mabadiliko ya sheria hiyo ili kuwezesha kutengeneza mazingira rafiki kwa watoto wakike mtoto kuweza kutimiza ndoto zao.

Askofu Mameo ameishauri jamii kuacha tabia ya kubadilisha mazao na binadamu kwa lengo la kuolewa na kwamba watoto wa kike waachwe wasome watimize ndoto zao zitakazowawezesha kulitumikia vyema taifa.
“Watoto wakike hapaswi kuuzwa kama mazao,kwani wana haki ya kupata haki zote ndani ya jamii ikiwemo elimu.” amesema Askofu Mameo.

Naye Sheikh wa Mkoa wa Morogoro, Twaha Kilango amesema ukatili wa kijinsia umeteketeza jamii kubwa ya watanzania,hivyo ifikie wakati tuungane pamoja na kuweka nguvu katika kutokomeza ukatili wa kijinisia hususani kupinga ndoa za utotoni katika jamii zetu.

“Tushikamane, tushirikiane na kupaza sauti katika kutokomeza ukatili kwa watoto wetu wa kike, wakati unabadilika na sisi tunapaswa kubalika, na tutumie viongozi wa dini katika kuelimisha jamii kwa uwazi ili kuibadilisha iondokane na mitazamo ambayo sio sahihi.”amesema Sheikh Kilango.

Naye chifu wa kabila la Kimasai, Kashu Moreto amesifu namna jamii za kifugaji zinavyobadilika kwa kuondokana na mila kandamizi hasa kwa wanawake na watoto wakike.

Amesema mabadiliko hayo yamechangiwa na elimu ambayo inayotolewa kwenye makanisa, misikitini na kwenye jamii inayohumiza wazazi kuwapeleka watoto shule huku akiwataka wazazi kukaa karibu na watoto kujua changamoto zao.

Kwa upande wake kiongozi mkuu wa mradi huo uliopo ndani ya kanisa hilo, Patricia Mwaikenda amesema mradi umekijita katika kufanya mabadiliko katika mila, desturi potofu ndani ya jamii ambazo zinamkandamiza mtoto wa kike kushindwa kutimiza malengo yake.

Mwaikenda ametaja malengo matatu ya mradi huo ni kuwajengea uwezo watoto wa kike kuweza kujitambua na kutoa taarifa pindi wanapofanyiwa ukatili, elimu kwa viongozi wa dini na utetezi wa mabadiliko ya sera na sheria ikiwemo sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Awali, baadhi ya watoto wakike walioshiriki maadhimisho hayo kwa nyakati tofauti wameeleza namna wanavyokabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukatili wa kijinsia nyumbani, shuleni na mitaani.

Wamesema pia baadhi yao kunyimwa fursa sawa ya kupata elimu ili kutimiza ndoto zao, kutothaminiwa hata kufikia hatua ya kulinganishwa thamani na ng’ombe, na kulazimishwa kuolewa katika umri mdogo ili wazazi waweze kupata mali hususani ng’ombe.

Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 haitoi utetezi wa haki ya mtoto wa kike kwa kuwa inahalalisha mtoto wa kike kuolewa akiwa na umri wa miaka 14 kwa ridhaa ya wazazi.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
6 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work AT Home
Work AT Home
1 month ago

I am making $100 an hour working from home. I never imagined that it was honest to goodness yet my closest companion is earning $16,000 a month by working on a laptop, that was really dumbfounding for me, she prescribed for me to attempt it simply. Everybody must try this for this job now by just using

this site link… http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
Gloria Tinsley
Gloria Tinsley
Reply to  Work AT Home
1 month ago

I work from home and earn a respectable $6k a week, which is amazing considering that a year ago I was unemployed in a terrible economy. I always give God praise for honoring me with these rules, and now it’s my duty to practice anticipatory compassion and share it with everyone. Likewise,

Here is I begun—> http://Www.Easywork7.com

Last edited 1 month ago by Gloria Tinsley
KILLER
KILLER
1 month ago

Utaongea mwenyewe kuwa KAFA LAKINI ALIJENGA GOROFA MTAA WA SABA – HISTORIA YAKE TAYARI IMEANDIKWA 2023..
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
MAANA YAKE KUFA KWA NGOMA AU MUUWAJI ANA MAANA/NGUVU/MAONO KULIKO RAIS TUSHIRIKISHE HISTORIA YAKO TAFADHARI!!!!!!!!?.

MargieHolland
MargieHolland
Reply to  KILLER
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by MargieHolland
KILLER
KILLER
1 month ago

Utaongea mwenyewe kuwa KAFA LAKINI ALIJENGA GOROFA MTAA WA SABA – HISTORIA YAKE TAYARI IMEANDIKWA 2023..
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
MAANA YAKE KUFA KWA NGOMA AU MUUWAJI ANA MAANA/NGUVU/MAONO KULIKO RAIS TUSHIRIKISHE HISTORIA YAKO TAFADHARI!!!!!!!!?…

KILLER
KILLER
1 month ago

*********TULIZANI TUPO TAYARI KUISHI……

DOWNLOAD HAPA UAPATE NGUVU ZA KIUME

Back to top button
6
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x