Viongozi wananufaika migogoro ya ardhi

MOROGORO; Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amesema migogoro mingi ya ardhi ndani ya mkoa huo ina sura mbaya,ni ya kutengenezwa na wapo watu wakiwemo viongozi wananufaika na migogoro hiyo kimyakimya.
Hivyo amewaagiza wakuu wa wilaya kufanya tathimini ya migogoro ya ardhi katika maeneo yao ambayo wataisimamia na itaratibiwa na wakurugenzi wa kila halmashauri, ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.
Malima ametoa maagizo hayo kwenye kikao na wakuu hao wailaya na wakurugenzi, ambacho kilihusu mwelekeo wa mkoa baada ya yeye kufanya ziara kila wilaya na kuona shughuli mbalimbali ndani ya kipindi cha miezi mitatu tangu alipokabidhiwa mkoa huo.
“ Nimepata heshima ya kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, nimepata muda wa kuona mambo mbalimbali nimefanya ziara ya kujitambulisha na nyingine ya kupitia hoja za CAG na tulikubaliana mambo kadhaa na kukaa kwangu kwa miezi hii mitatu ,tunaona bado hatuendi vizuri sana, “ amesema Malima.
Ameyataja mambo matatu ambayo hayaendi vizuri sana ni kuwepo kwa migogoro ya ardhi iliyokithiri , migogoro ya wafugaji na wakulima pamoja na migogoro baina ya viongozi wenyewe kwa wenyewe.
“ Lakini katika hili lazima tukubaliane ya kwamba migogoro ya ardhi ya Morogoro mingi ni ya kujitakia wenyewe …nimejipa muda wa miezi mitatu kukaa kama mkuu wa mkoa wa Morogoro na kuyaelewa na kuyasoma, lakini mingi ni migogoro ya kujitakia, “ amesema.
Amesema kuwa, wapo viongozi kwenye ngazi za vitongoji , vijiji na kata ambao ni chanzo cha kutengeneza hiyo migogoro.
“ Nataka niseme kwa kweli kati hili masuala ya migogoro ya ardhi , nimeliangalia na nimebaini migogoro mingi ni ya kutegeneza hasa kwa viongozi sisi wenyewe, “ amesema Malima
Kutokana na uzito wa jambo hilo amemtaka kila mkuu wa wilaya na kamati yake ya usalama kwenda kufanya tathimini ya migogoro ya ardhi katika maeneo yao na kuwasilisha taarifa kwake ili hatua ziweze kuchukuliwa.
“ Tunakuwa na migogoro ambayo inatengenezwa na watu , harafu inasambaa na kuleta sifa mbaya kwenye mkoa wetu wa Morogoro “ amesema Malima.
★Join this most wonderful and cool online home based job and start making more than $700 every day. I made $24583 last month, ( a11q) which is incredible, and I strongly encourage you to join and begin earning money from home. Simply browse to this website now for more information.
Click and Copy Here══════►►► http://Www.SmartCareer1.com
I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com
Mashindano ya nani kuhinda kwenye neno “ABROAD“ NCHINI TANZANIA!?
MJERUMANI
MHINDI
MTANZANIA
MKENYA
MNIGERIA
MHISPANIA
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
NANI AINGIZE NDEGE ZA KWENDA KUMSALIMIA BABU NA BIBI, KWA ALIYESHINDA KULELEWA NA BIBI TU!?