Waahidi kutunza misitu kuinua uchumi

MANYARA; Jamii ya Wahadzabe, Wadatoga na Masai kutoka Wilaya za Mbulu na Kiteto mkoani Manyara wamesema wataendelea kulinda na kutunza misitu ya asili kama njia mbadala ya kuinua uchumi wao.

Kauli hiyo imetokana na jamii hiyo kupata Sh bilioni 4 za biashara ya hewa ya ukaa ikiwa ni matokeo ya utunzaji wa misitu ya asili na mazingira.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Selemani Jaffo, alikabidhi mfano wa hundi ya Sh bilioni 4.7 kutoka kwa kampuni ya Carbon Tanzania, ikiwa ni malipo ya fedha za uuzaji wa hewa ya ukaa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Whiterose Babati.

Wanufaika hao wanatoka Vijiji vya Yaeda Chini na Makame vilivyopo Halmashauri za Wilaya ya Mbulu na Kiteto.

General Mathias, mnufaika kutoka jamii ya Wahadzabe alibainisha kuwa maisha ya Wahazabe, Wamasai na Wagatoga yanategemea misitu ya asili kwa ajili ya kurina asali na uwindaji.

“Tunaishukuru  Kampuni ya Carbon kwa kuwa inalinda misitu ya asili na imetupa elimu ya kuacha kukata misitu hovyo  na kuchoma moto kurina asali, kampuni ni rafiki wa kwetu pia,” amesema Mathias.

Waziri Jaffo amewaasa wananchi kuendelea kuiamini serikali yao kutokana na ahadi na mipango ya maendeleo inayotekeleza.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara,  Queen  Sendiga alieleza kuwa fedha zilizotolewa zitasaidia kusomesha watoto kuanzia elimu ya msingi hadi vyuo vikuu na kujenga zahanati vituo vya afya na kurekebisha miundo mbinu ya Barabara.

NaYe Mkurugenzi wa fedha Kampuni ya Carbon Tanzania,  Alphael Jackson aliwahakikishia wananchi hao kuendelea kutoa fedha ikiwa utunzaji wa mazingira utakuwa endelevu.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JELA LA NJE
JELA LA NJE
23 days ago

Sehemu Salama KUTAFUTA NA KUPATA wanawake wazuri wa KUOA NA kulea WATOTO NA KUZAA WATOTO KATIKA MIAKA 200 IJAYO NI CHATO

KABILA ALIKOTOKA JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI – HAKIKA WAMEMALIZA ICE-CREAM YOTE, WANAHAMU YA KUTOA RAIS MWINGINE KWA MIHULA 20 IJAYO.

MAKABILA MENGINE YOTE NDOTO ZA KUTOA URAIS KWENYE MIHULA IJAYO ZIPO KWA ASILIMIA 200- UTAPIGWA JELA LA NJE

Capture.JPG
EliseMcGhee
EliseMcGhee
23 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 23 days ago by EliseMcGhee
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x