KAMATI za kudumu za Bunge za Nishati na Madini, pamoja na ya Bajeti zimewasili mkoani Mtwara leo kwa ajili ya ziara ya siku moja kutembelea miundombinu ya kuchakata gesi asilia Madimba, visima vya gesi MnaziBay na miundombinu ya kupokea mafuta Bandari ya Mtwara.
Kamati ya Nishati na Madini inatembelea miundombinu ya kuchakata gesi asilia Madimba na visima vya gesi MnaziBay, wakati Kamati ya Bajeti, inatembelea miundombinu ya kupokea mafuta Bandari ya Mtwara.
Baada ya ziara hiyo kamati hizo zitaendelea na ziara nyingine, ambapo Kamati ya Nishati na Madini itatembelea mradi wa Julius Nyerere na kamati ya bajeti itatembelea mradi wa bomba la mtafuta Afrika Mashariki (EACOP).