Wachezaji 12 nje United ikiikabili Bayern

MENEJA wa Manchester United, Erik ten Hag anasem “hajawahi kuanzisha kikosi chake bora zaidi” huku timu yake iliyokumbwa na majeraha ikijiandaa kukabiliana na Bayern Munich michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

United itawakosa wachezaji 12 wa kikosi cha kwanza.

Wachezaji hao ni Raphael Varane, Mason Mount na Harry Maguire, ambao hawajasafiri kwenda Munich.

“Nadhani sikuwahi kuanzisha kikosi bora yote unatakiwa kukabiliana nayo. Napenda hali hizi. Unapaswa kujua nini cha kufanya na kuzingatia mchakato.”

Beki Varane na kiungo Mount wote walishiriki mazoezi Carrington Jumanne asubuhi ili kuongeza matumaini ya kurejea kwenye mchezo wa ufunguzi wa Kundi A, ambalo pia linajumuisha Galatasaray ya Uturuki na FC Copenhagen kutoka Denmark.

Varane amekosa mechi mbili zilizopita na Mount tatu, huku United wakianza vibaya msimu wa Ligi Kuu, wakipoteza michezo mitatu kati ya mitano ya kwanza.

Beki wa kati Maguire pia alifanya mazoezi Jumanne, lakini alipata jeraha ambalo lilimfanya kuwa nje.

Ten Hag pia anawakosa washambuliaji Antony na Jadon Sancho, ambao hawafanyi mazoezi na kikosi kwa sasa, pamoja na kiungo wa Uholanzi Donny van de Beek, ambaye hajasajiliwa kwa michezo ya Ulaya.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
KYLEXY
KYLEXY
2 months ago

Balozi wa Canada anatafuta vijana 6,500,000 kwa ajili ya kuandaa KIJIJI cha UJAMAA nchini Canada (KYLE XY).. Kama umesoma kuanzia level ya form six HADI PHD

Capture.JPG
KYLEXY
KYLEXY
2 months ago

Balozi wa Canada anatafuta vijana 6,500,000 kwa ajili ya kuandaa KIJIJI cha UJAMAA nchini Canada (KYLE XY).. Kama umesoma kuanzia level ya form six HADI PHD…

Capture.JPG
Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x