Wachimbaji madini watakiwa kutunza mazingira

MKUU  wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Joseph Mkude amewataka Wananchi wanaofanya shughuli  za kibinadamu na uchimbaji wa madini kwenye eneo la Hifadhi la Bwawa la Songwa waache mara moja na kuendelea kutunza mazingira na vyanzo vya maji.

Mkude aliyasema hayo Novemba 13, 2023 wakati akizindua uwekaji wa bikoni katika eneo  bwawa hilo  na kupanda miti ambapo alisema wafugaji  na wachimbaji wadogo wamekuwa chanzo cha uhalibifu  wa mazingira kwenye bwawa hilo.

Advertisement

Alisema mazingira mazuri yanatakiwa kutunzwa kwani mmepata bahati ya kuwa na mabwawa mawili ni vyanzo vizuri kwa matumizi ya nyumbani na kilimo hivyo ni lazima tuyawekee mipaka ili Wananchi wasivamie.

“Rais  wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  anasisitiza uhifadhi wa mazingira na kishapu ni kame na  Kampuni ya Mgodi wa Almas wa  Wiliamson Diamond  LTD  imekuwa ikijitahidi kuzalisha miche na kuigawa bure”alisema Mkude.

Mkude alisema zoezi la kuweka  mipaka limefanyika  kwa lengo la kuhifadhi chanzo cha maji  kisiingiliwe na mifugo wala kushughuli za kilimo ikiwemo uvuvi haramu  wapo  baadhi ya Wananchi walikuwa wakikataa kupanda miti sasa wameelewa na zoezi la upandaji limeenda vizuri.

Diwani wa kata ya Songwa Abdul Ngoromole alisema  changamoto  iliyokuwa ikijitokeza kwenye bwawa hilo kina cha maji kikipungua Wananchi wanaanza  kugeuza maeneo ya kandokando kuwa eneo la kilimo na wachimbaji  wadogo kuvamia wakidhani kuna almas.

“Maeneo mengi yamechibwa ndiyo maana ofisi za bonde la maji la kati wamekuja na kuweka bikoni  na kutoa onyo kwa watakao halibu mazingira lakini sisi viongozi wa maeneo haya tutahakikisha tunalinda hifadhi”alisema Ngoromole.

Mwenyekiti wa kijiji cha Songwa Damas Francis alisema kijiji hicho kina wakazi 2559  ambapo alisema wako tayari kutunza na kulinda  vyanzo vya maji ili visipoteze ikolojia iliyokuwepo

Mwenyekiti wa jumuiya ya watumia maji kijiji cha Songwa Zainabu Issa alisema wamekuwa wakipeana elimu juu ya utunzaji wa mazingira na maji hayo yamekuwa yakiwafaidisha kipidi cha kiangazi nakuondoa shida ya maji.

Mhandisi mazingira kutoka bonde la maji  la kati Nyacheri Mramba alisema  bikoni zilizowekwa ni 402  na tanki  mbili zimejengwa kwaajili ya kunyweshea  mifugo  bila kuathiri  mazingira  ya bwawa pia watu wamekuwa wakilima na kuchimba madini  kando ya bwawa jambo ambalo ni hatari itasababisha bwawa kukauka.

1 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *