Wafanyakazi Wapalestina kurudishwa Gaza

TEL-AVIV, Israel MAELFU ya wafanyakazi wa Kipalestina waliokuwa Israel watarejeshwa Gaza, imeeleza taarifa ya Redio ya Jeshi la Israel.

Imeripotiwa zaidi ya mabasi 10 yameelekea kivuko cha Kerem Shalom yakiwa na wafanyakazi 300 na takriban 1,000 watahama kesho.

GLZ Redio ilisema wafanyakazi hao walikamatwa awali na kuwekwa kizuizini kwa vile walikuwa wakiishi nchini kinyume cha sheria.

Advertisement

Tangu Oktoba 7, Israel imerudia mara kadhaa kurudisha maelfu ya Wapalestina kwenye eneo lililozingirwa, ikifuatilia ukandamizaji dhidi ya wafanyikazi na vibarua kutoka eneo hilo ambao hapo awali walikuwa wamepewa vibali vya kuchukua kazi nchini Israeli na Ukingo wa Magharibi unaokaliwa.

Hapo awali Israel ilikuwa imetoa vibali zaidi ya 18,000 vinavyowaruhusu Wagaza kuvuka kuingia Israel na Ukingo wa Magharibi kufanya kazi katika sekta kama kilimo au ujenzi ambazo kwa kawaida hulipa mishahara hadi mara 10 ya ile ambayo mfanyakazi angeweza kulipwa katika Ukanda wa Gaza

4 comments

Comments are closed.

/* */