Wafugaji wakorofi kutengwa

WIZARA ya Mifugo na Uvuvi imesema haitawaunga mkono wafugaji wakorofi na wasiofuata sheria zinazosimamia matumizi bora ya ardhi na watakao kusababisha migogoro baina yao na watumiaji wengine wa ardhi wakiwemo wakulima.
Naibu Waziri wa Wizara hiyo , Alexander Mnyeti amesema hayo wilayani Mvomero kwenye halfa ya uzinduzi wa kampeni ya Tutunzane Mvomero 2023 iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima.
Mnyeti amesema baadhi ya wafugaji wamekuwa wakitumia uwezo wao wa kifedha kutoa rushwa kwa baadhi ya watoa maamuzi wanapofikishwa kwenye vyombo vya haki licha ya mkulima kupata hasara ya mazao yake kuliwa mifugo huonekana ndiye mkosaji na kushindwa kupata haki yake.
“Wizara ya Mifugo na Uvuvi tumeamua kusimamia ukweli na sheria hatutakuwa tayari kumtetea mfugaji atakayevunja sheria na kuingiza mifugo kwenye mashamba ya wakulima kwani kumtetea ni kuchochea migogoro ndani ya wilaya Mvomero na maeneo mengine nchini .”amesema Mnyeti.
Mnyeti amesema watoa maamuzi kutenda haki na kuepuka rushwa ili migogoro iliyopo Mvomero na maeneo mengine nchini itoweke na amani kwa jamii zote mbili itawale.
“Ni kweli kuwa baadhi ya wafugaji ni wakorofi na wamekuwa wakiingiza mifugo yao kwenye mashamba ya wakulima kwa makusudi jambo ambalo halikubaliki.”amesema Mnyeti
Amesema ni vyema wafugaji wa wilaya ya Mvomero na nyingine ndani ya mkoa huo kufuga mifugo yenye tija kwa taifa na kujiepusha kutumia fedha walizo nazo kuwanyanyasa wakulima.
“ Wafugaji fungeni mifugo yenye tija kwa Taifa, kulima mashamba ya malisho pamoja na kuchimba visima vya kunyweshea mifugo. “ amesisitiza Mnyeti.
Mnyeti amesema kwa kufanya hivyo kutachangia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto ya migogoro ya ardhi wilayani Mvomero na maeneo mengine nyakati za kiangazi.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mvomero, Judith Nguli amesema kampeni ya Tutunzane Mvomero 2023 imelenga kuleta ushirikiano ,umoja ,upendo na mshikamano baina ya wakulima na wafungaji hali ambayo itasaidia kwa kiwango kikubwa kuondoa migogoro.
NEC UCHANGUZI LEO
Nani anafaa KUWA RAIS wa Tanzania mzungu kulipa fadhila za OBAMA KUWA RAIS WA MAREKANI NA Greg Fergus SPIKA WA CANADA WA SASA!? – Hongera kwa kuzaa kizazi kisichojihusisha na SIASA
NEC UCHANGUZI LEO
Nani anafaa KUWA RAIS wa Tanzania mzungu kulipa fadhila za OBAMA KUWA RAIS WA MAREKANI NA Greg Fergus SPIKA WA CANADA WA SASA!? – Hongera kwa kuzaa kizazi kisichojihusisha na SIASA…
NEC UCHANGUZI LEO
Nani anafaa KUWA RAIS wa Tanzania mzungu kulipa fadhila za OBAMA KUWA RAIS WA MAREKANI NA Greg Fergus SPIKA WA CANADA WA SASA!? – Hongera kwa kuzaa kizazi kisichojihusisha na SIASA/
NEC UCHANGUZI LEO
Nani anafaa KUWA RAIS wa Tanzania mzungu kulipa fadhila za OBAMA KUWA RAIS WA MAREKANI NA Greg Fergus SPIKA WA CANADA WA SASA!? – Hongera kwa kuzaa kizazi kisichojihusisha na SIASA?
Earn money in USA, high scores from trusted resources. Work at your own pace. Regular Payments. Search in different job categories. Work anywhere on your vs03 computer, laptop or mobile phone. Update your profile at any time.
.
.
Detail Here———->>> http://Www.Smartcash1.com