Wafugaji watakiwa kuhifadhi malisho

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Idara ya Mifugo), Tixon Nzunda (wa tatu kushoto), akikagua malisho ya mifugo katika Taasisi ya utafiti TALIRI Mpwapwa(Picha na Sifa Lubasi).

WAFUGAJI nchini wametakiwa kuwa na utamaduni wa kuhifadhi malisho, ili kuweza kukabiliana na ukame unaotishia kuua mifugo.

Kauli hiyo imetolewa  na Katibu  Mkuu  wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Idara ya mifugo  Tixon Nzunda, wakati wa ziara ya kutembelea  Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TARILI) na Taasisi ya Wakala wa Mafunzo ya Mifugo   (LITA), kampasi ya Mpwapwa.

Nzunda aliwataka wafugaji kuwa na utamaduni wa kuhifadhi malisho ili kukabiliana na ukame.

Advertisement

Pia amezitaka taasisi zote za utafiti wa mifugo kuongeza kasi ya uzalishaji na uvunaji wa majani ya malisho,  ambayo yatauzwa kwa wananchi, ili kuweza kutunza mifugo yao na kupata tija katika ufugaji wao.

Akizungumzia mradi wa uzalishaji wa ndama kwa kutumia viini tete, alisema wakati serikali inajipanga kuondoa changamoto zilizopo, lazima kuanza kufanya kile kinachowezekana kufanyika kwa kutumia raslimali zilizopo.

Kwa upande wake, Mtalaam wa kitengo cha maabara ya uzalishaji Kwa kutumia viini tete, Kabun Thomas alisema  tayari wamefanikiwa kuzalisha ndama mmoja, ambaye ametokana na viini tete hivyo.

Alisema kuwa  ili kukamilisha vifaa vyote vilivyobaki, taasisi hiyo inahitaji jumla ya Sh  milioni 800, ili kukamilisha vifaa vyote vya kuvunia  kugandishia na kuhifadhia, ili kuleta tija katika mradi huo.

 

 

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *