Wajivunia Tamasha la Serengeti Lite

DAR ES SALAAM: ZAIDI ya wajasiriamali 500 wamenufaika na  fursa za kibiashara kwa kuuza bidhaa mbalimbali pamoja na kutengeneza mtandao kupitia wadau kutoka Kanda ya Afrika Mashariki na Kati walioshiriki Tamasha la Serengeti Lite jana Fukwe za Coco, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika tamasha hilo, Meneja Mawasiliano  na Uendelevu Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Rispa Hatibu, amesema kuwa licha tamasha kutoa burudani kupitia kwa wasanii kutoka  ndani na nje ya nchi, pia  limekusudia kuinua vipato vya wajasiriamali wadogo katika kuuza bidhaa pamoja na kujitangaza.

Advertisement

Nao baadhi ya wajasiriamali walioshiriki katika tamasha hilo wamesema kuwa ni fursa ya kipekee ambayo wameipata ya kujitangaza, huku wakitoa  wito kwa wadau wa maendeleo kuendelea kuwashirikisha kushiriki katika  matamasha mengine kwa ajili kufungua kutafuta fursa za kibiashara.

2 comments

Comments are closed.