Wakandarasi wazawa wafundwa

WAKANDARASI wazawa wametakiwa kuzisimamia kampuni zao kwa ufasaha kwa kufuata sheria za manunuzi ya umma.

Pia, wametakiwa kulipa kodi kwa wakati na kufanya kazi kwa weledi kwa kutumia wataalamu stahiki katika sekta mbalimbali ili kukwepa changamoto katika maeneo yao ya kazi.

Akizungumza katika mafunzo yaliyofanyika kwa siku tatu yenye lengo la kuwajengea uwezo Makandarasi wazawa kibiashara, jijini Dar es salaam, Msajili wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Rhoben Nkori, amesema  lengo moja wapo ni kutoa elimu kwa makandarasi kuhusiana na mfumo mpya wa manunuzi kwa Umma (Nest).

“Hii inatokana na kuwa na mabadiliko makubwa ya sheria ya manunuzi ya umma na tayari sheria ipo katika hatua za mwisho kabla haijawa sheria kamili.”Amesema na kuongeza

“Biashara ya Ukandarasi ni kubwa na kuanzia mwanzo ni unaingia kwenye mifumo inayostahili na unadhibitiwa. Mifumo ya CRB ni miongoni iliyounganishwa na Nest na mkandarasi hatoweza kufoji wala kudanganya chochote pale atakapokua anaingiza taarifa zake”, amesema Msajili.

Amesema, wakandarasi wabadilishe mtazamo wao na kuwa wafanyabiashara wa kweli na halali bila kukwepa kulipa kodi, kufoji nyaraka na kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia sheria za nchi.

Aidha Nkori, amesema makampuni mengine hutumika kufanya kazi kwa majina ya wamiliki wengine yanayopelekea mvutano pindi kazi inapoenda kukaguliwa na TRA kupitia Bodi ya Usajili wa Makandarasi(CRB) hivyo amewataka wamiliki wa makampuni kusimamia vyema makampuni yao ili kuepuka changamoto hizo.

Nkori amesisitiza kuwa ili kuendelea kujenga taswira nzuri kwa wakandarasi nchini, Bodi itaendelea kuwachukulia hatua kisheria wakandarasi wote wanaokiuka maadili yao ya kazi.

 

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JessicaRobertson
JessicaRobertson
17 days ago

Single Mom With 4 Kids Lost Her Job But Was Able To Stay On Top By Banking Continuously DOLLER 1500 Per Week With An Online Work She Found Over The Internet… 

Check The Details HERE…..  https://earncash82.blogspot.com/

Last edited 17 days ago by JessicaRobertson
Nadine Taylor
Nadine Taylor
13 days ago

I make over 13k a month working part-time. I listened to different humans telling me how a good deal of cash they may make online,N255 so I was determined to locate out. Well, it turned into all actual and it absolutely modified my life. Everybody must try this job now

by just using this site….. http://bigmoney8.store

Royal
12 days ago

My last salary was $8750, ecom only worked 12 hours a week. My longtime neighbor kl estimated $15,000 and works about 20 hours for seven days. I can’t believe how blunt he was when I looked up his information,copy and open it……….. http://www.works75.com

Last edited 12 days ago by Royal
Next King of Tanzania
Next King of Tanzania
10 days ago

“JENGA UKIFA UTAZIACHA NA WATOTO WENU WATAUZIUZA” BY SAMIA SULUHU HASANI

 

HIVI MWANADAMU AKIFA HUWA AACHA NINI KULE BY TULIA AKSON

AKUTA NYOKA KWENYE VIATU VYAKE, AUMWA NA KUFA HAPO HAPO

HATA UTARATIBU TULIOUJENGA INABIDI TUFE TUUACHE WAKITAKA WAKUUZE ULAYA

Capture.JPG
Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x