Wakulima washauriwa kukata bima ya mazao

WAKULIMA  nchini wameshauriwa kukata Bima ya mazao ili iwakinge na maafa  mbalimbali na kuwapa uhakika na usalama wa shughuli zao kabla na baada ya kupata maafa yatokanayo na changamoto za kilimo.

Afisa Bima wa NIC Insurance Experius Nchanila  akiongea na HabariLeo katika Maonyesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara ‘Sabasaba’ katika Banda la NIC amesema NIC  imeanzisha bima hiyo ya kilimo kwa vile kilimo ni fursa ya ajira, kilimo ni chakula, inatoa mali ghafi katika viwanda na inachangia asilimia 28 ya pato la taifa.

“Kilimo ni uti wa mgongo,  asilimia kubwa ya watanzania wanategemea kilimo.”Amesema Nchanila na kuongeza

“Hata hivyo, Kilimo kimezungukwa na changamoto nyingi ikiwa za majanga yasiyoepukika, mfano mafuriko, moto, ukame, wadudu, wanyama wasiodhibitika, hivi vyote uathiri zaidi kilimo.”Amesema

|Amesema, kupitia changamoto hizo, wakulima wengi wamekuwa wakipata tabu na kupoteza mitaji yao, wanashindwa kupata kilimo chenye tija.

“Sasa NIC insurance imekuja na suluhisho la majibu kwa kuwaletea bima ya kilimo, inakinga majanga yote, inamuhakikishia mkulima anapowekeza pesa yake na nguvu kazi  aliyoweka kwenye kilimo haiwezi kupoteza.”Amesema

Aidha, amesema vigezo vya kukata bima hivyo ni kuwa na vielelezo ambavyo vinaonyesha  umiliki halali wa shamba, awe anazingatia taratibu za kilimo, historia ya eneo hilo au shamba alilokatia bima, historia ya hali ya hewa ya eneo hilo na aeleze ni zao gani ambalo analikatia bima.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Eleanor J. Gonzalas
Eleanor J. Gonzalas
2 months ago

I earn 200 dollars per hour working from home on an online job. I never thought I could accomplish it, but my best friend makes $10,000 per month doing this profession and that I learn more about it.
.
.
.
For Details►—————————➤  http://www.pay.hiring9.com

Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x