Wanahabari wapatiwa elimu usimamizi wa maadili

WAANDISHI wa habari wanawake zaidi ya 116 wamepata mafunzo ya menejimenti ikiwemo usimamizi wa maadili na ushirikiano kwenye vyombo vya habari Tanzania Bara na Visiwani.

Akifungua mafunzo ya siku tatu yanayofanyika jijini Arusha na kushirikisha waandishi wa habari wanawake, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzani (MCT), Kajubi Mukajanga amesititiza wanahabari wanawake wanapaswa kuwa viongozi wenye maamuzi ya kusimamia vyema maadili ya vyombo vya habari.

“Waandishi wa habari wanawake ni viongozi wazuri endapo vyumba vyao vya habari vikiwapa nafasi pasipo kubaguliwa ingawa tunajua vyombo vingi vya habari vinaongozwa na wanaume lakini tunasisitiza pia wanawake wanahabari wapate nafasi za uongozi.” Amesema Mukajanga

Naye mmoja kati ya wakufunzi mkongwe katika tasnia ya habari, Pili Mtambalike amesema uongozi bora ni ushirikiano baina ya waandishi wa chini na wahariri katika kuhakikisha kazi zinazofanywa zinafanyika kwa usahihi sanjari na mabosi kuthamini kazi zinazofanywa na wanahabari kwa kuwashukuru.

Ameongeza pia ni lazima wanahabari wanawake wakawa wabunifu katika uboreshaji wa kazi zao wanazosimamia ikiwemo kujali maslahi ya wanahabari wengine wanaowaongoza na kutambua mchango wa kila mtu katika tasnia ya habari pamoja na kugatua madaraka ili hata mhusika atakapoondoka kunamtu anaweza kusimamia kazi mbalimbali ili ziende.

MCT imetoa mafunzo ya wanahabari wanawake katika masuala ya uongozi ikiwemo rasilimali fedha na sheria mbalimbali tangu mwaka 2019 na wanahari mbalimbali wamenufaika katika mikoa ya Morogoro,Dar es Salaam, Tanga, Zanzibar, Moshi na sasa Mkoa wa Arusha.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
neknoyirze
neknoyirze
3 months ago

 [๐‡๐จ๐ฐ ๐“๐จ ๐Œ๐š๐ค๐ž ๐„๐ฑ๐ญ๐ซ๐š ๐ˆ๐ง๐œ๐จ๐ฆ๐ž ๐…๐ซ๐จ๐ฆ ๐‡๐จ๐ฆ๐ž ๐‚๐ก๐š๐ง๐ ๐ž ๐˜๐จ๐ฎ๐ซ ๐‹๐ข๐Ÿ๐ž ๐๐Ž๐–]ๅฝกโ˜…

 ๐†๐จ๐จ๐ ๐ฅ๐ž ๐ข๐ฌ ๐ฉ๐ซ๐ž๐ฌ๐ž๐ง๐ญ๐ฅ๐ฒ ๐ฉ๐š๐ฒ๐ข๐ง๐  $๐Ÿ๐ŸŽ,๐Ÿ’๐Ÿ’๐Ÿ• ๐ญ๐จ $๐Ÿ๐Ÿ‘,๐ŸŽ๐Ÿ๐Ÿ“ ๐ž๐ฏ๐ž๐ซ๐ฒ ๐ฆ๐จ๐ง๐ญ๐ก ๐Ÿ๐จ๐ซ ๐ฐ๐จ๐ซ๐ค๐ข๐ง๐  ๐จ๐ง ๐ญ๐ก๐ž ๐ฐ๐ž๐› ๐Ÿ๐ซ๐จ๐ฆ ๐ก๐จ๐ฆ๐ž. ๐ˆ ๐ก๐š๐ฏ๐ž ๐ฃ๐จ๐ข๐ง๐ž๐ ๐ญ๐ก๐ข๐ฌ ๐š๐œ๐ญ๐ข๐ฏ๐ข๐ญ๐ฒ ๐Ÿ ๐ฆ๐จ๐ง๐ญ๐ก๐ฌ ๐›๐š๐œ๐ค ๐š๐ง๐ ๐ˆ ๐ก๐š๐ฏ๐ž ๐ž๐š๐ซ๐ง๐ž๐ $๐Ÿ๐Ÿ“,๐Ÿ๐Ÿ’๐Ÿ– ๐ข๐ง ๐ฆ๐ฒ ๐Ÿ๐ข๐ซ๐ฌ๐ญ ๐ฆ๐จ๐ง๐ญ๐ก ๐Ÿ๐ซ๐จ๐ฆ ๐ญ๐ก๐ข๐ฌ ๐š๐œ๐ญ๐ข๐ฏ๐ข๐ญ๐ฒ. ๐ˆ ๐œ๐š๐ง ๐ฌ๐š๐ฒ ๐ฆ๐ฒ ๐ฅ๐ข๐Ÿ๐ž ๐ข๐ฌ ๐ข๐ฆ๐ฉ๐ซ๐จ๐ฏ๐ž๐ ๐ญ๐จ๐ญ๐š๐ฅ๐ฅ๐ฒ!
.
.
๐‹๐จ๐จ๐ค ๐š๐ญ ๐ข๐ญ ๐ฐ๐ก๐š๐ญ ๐ˆ ๐๐จ—————————->> http://www.join.hiring9.com

Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x