Wanajeshi walinda amani 15,000 kuondoka Congo

UJUMBE wa Umoja wa Mataifa wa kuleta amani nchini DR Congo (MONUSCO) umetia saini mkataba wa kuwaondoa wanajeshi 15,000 wa kulinda amani nchini humo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa taifa hilo, Christophe Lutundula na Mkuu wa Monusco wametiliana saini makubaliano hayo Jumanne Novemba 21, 2023.

Katika mazungumzo yake na televisheni ya taifa, Lutundula amesema mpango huo unaashiria kufika mwisho wa ushiirikiano.

Wakati hayo yanajiri, wiki iliyopita Serikali ya Congo iliagiza jeshi la Kanda ya Afrika Mashariki kuondoka nchini humi ifikapo Disemba mwaka huu.

3 comments

Comments are closed.

/* */