Wananchi Iringa wapata ushauri wa kisheria bure

WANANCHI wasio na uwezo wa Manispaa ya Iringa na vitongoji vyake wamejitokeza katika viwanja vya Bustani ya manispaa hiyo kupata msaada wa ushauri wa kisheria unaotolewa bure na Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) Kanda ya Iringa.

Mawakili wa kujitegemea zaidi ya 50 ambao ni wanachama wa chama hicho watakuwepo katika viwanja hivyo leo na kesho kufikisha huduma hiyo kwa wenye uhitaji.

Mwenyekiti wa kanda hiyo , Moses Ambindwile amesema; “Tunawakaribisha wananchi wote wanaohitaji msaada wa kisheria katika masuala yote ikiwemo mirathi, ndoa, ardhi na biashara.”

Ambindwile alisema ikiwa unastahili msaada wa kisheria, utapewa maelekezo kuhusu hatua inayofuata na usaidizi katika kesi yako au suala la kisheria.

Alisema ndani ya siku mbili, wanatarajia kutoa huduma hiyo kwa wananchi zaidi ya 100 na akawata waendelee kujitokeza.

Mwakilishi wa kampuni ya uwakili ya BLS, Barnabas Nyalusi amesema kampuni yao imedhhamini huduma hiyo ya ushauri wa kisheria ikitambua kwamba mahakama ni msingi muhimu wa mfumo wa kisheria na demokrasia.

Alisema kanda yao ina imani kubwa na mahakama na namna inavyofanya kazi bila kuingiliwa na mamlaka nyingine, ikiwa ni pamoja na serikali na hiyo ni muhimu kwa kutoa haki na kudumisha usawa na utawala wa sheria katika jamii.

Nyalusi alisema Uhuru wa mahakama unahakikisha kuwa kila raia anaweza kutafuta haki zake kwa imani katika mfumo wa kisheria.

“Kwahiyo tupo hapa katika viwanja hivi tunawasubiri wasio wenye uwezo na wanaohitaji msaada wa kisheria waje na changamoto zao za kisheria tuwasaidie kwa kuwapa msaada wa ushauri wa kisheria,” alisema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work AT Home
Work AT Home
1 month ago

I make $100h while I’m daring to the furthest corners of the planet. Last week I worked by my PC in Rome, Monti Carlo finally Paris… This week I’m back in the USA. All I do are basic tasks from this one cool site. see it, 

Copy Here→→→→→ http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
Gloria Tinsley
Gloria Tinsley
Reply to  Work AT Home
1 month ago

I work from home and earn a respectable $6k a week, which is amazing considering that a year ago I was unemployed in a terrible economy. I always give God praise for honoring me with these rules, and now it’s my duty to practice anticipatory compassion and share it with everyone. Likewise,

Here is I begun—> http://Www.Easywork7.com

Last edited 1 month ago by Gloria Tinsley
KILLER
KILLER
1 month ago

Utaongea mwenyewe kuwa KAFA LAKINI ALIJENGA GOROFA MTAA WA SABA – HISTORIA YAKE TAYARI IMEANDIKWA 2023..
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
MAANA YAKE KUFA KWA NGOMA AU MUUWAJI ANA MAANA/NGUVU/MAONO KULIKO RAIS TUSHIRIKISHE HISTORIA YAKO TAFADHARI!!!!!!!!?.

MargieHolland
MargieHolland
Reply to  KILLER
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by MargieHolland
KILLER
KILLER
1 month ago

Utaongea mwenyewe kuwa KAFA LAKINI ALIJENGA GOROFA MTAA WA SABA – HISTORIA YAKE TAYARI IMEANDIKWA 2023..
file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg
MAANA YAKE KUFA KWA NGOMA AU MUUWAJI ANA MAANA/NGUVU/MAONO KULIKO RAIS TUSHIRIKISHE HISTORIA YAKO TAFADHARI!!!!!!!!?..

Back to top button
5
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x