Waonywa uharibifu miundombinu ya umeme

WAKAZI wa Mkoa wa  Mwanza wametakiwa kuacha tabia ya uharibifu wa miundombinu ya Shirika la Umeme nchini (TANESCO).

Meneja wa shirika hilo mkoani hapa, Said Msemo amesema hayo wakati wa mahojiano maalum na mtandao wa HabariLEO.

Amesema mpaka sasa ni zaidi ya wateja wao 150 wameathirika na ubadhirifu wa miundombinu na kulipa hasara shirika hilo zaidi ya Sh milioni 151.

Advertisement

“hivi karibuni Kumeibuka changamoto ya wizi, ubadhirifu na uharibigu wa miundo mbinu ya Umeme na kulipa Shirika hasara Kwa kuiba,kuangusha na kuchukua mafuta ya Transfoma.” amesema Msemo.

Ameweka wazi kuwa  kuanzia mwezi Machi mpaka Juni mwaka huu shirika hilo limeishapoteza transfoma sita katika Wilaya za Magu, Kwimba na Misungwi.

Amesema upotevu wa transfoma hizo umesababisha baadhi ya wateja kukosa huduma hiyo na kusababisha Shirika hilo kukosa mapato  ya Sh milioni 9  kwa siku.

“Thamani ya Transfoma hizi zilizoibiwa peke yake ni  zaidi ya Sh milioni 51 na kama shirika ukiachilia mbali changamoto walizozipata hawa wateja  150  tumeweza kukosa mapato ya milioni 9 Kwa siku kwahyo ukijumlisha Transfoma na mapato haya ambayo tumekosa  tumepoteza zaidi ya milioni 60.” amesema Msemo

Amesema kuwa mpaka Sasa wanawashukiwa wanne wanaodhaniwa kuwa wameshiriki ubadhirifu huo huku wengine wakiendelea kusakwa. Msemo ametoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa shirika hilo kwa kulinda miundo mbinu hiyo.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *