Wapewa msaada wa magari programu za elimu

WIZARA  ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imepokea magari mawili yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 250 kutoka kwa Shirika la Maendeleo la Uingereza la UK-AID kwa ajili ya ufuatiliaji na tathimini ya shughuli za kielimu za Program ya shule bora nchini.

Makabidhiano hayo yamefanyika  leo Novemba 16, 2023 katika Ofisi za Taasisi ya Elimu Tanzania (TET)  jijini Dar es Salaam na kupokelewa na  Naibu Katibu  Mkuu wa WyEST, Franklin Rwezimula na  kuyakabidhi kwa Naibu Katibu OR -TAMISEMI Dk  Charles Msonde tayari kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Dk Rwezimula  ameishukuru UK-AID kwa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha Sekta ya Elimu kwa kutoa magari hayo yatayosaidia utekelezaji wa mradi huo.

“Tunashukuru kwa msaada huu, kwani utaimarisha ufuatiliaji  na tathimini katika miradi ya elimu  na umekuja wakati muafaka  kujua  utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili kubaini changamoto mbalimbali,” amesema Dk  Rwezimula.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, OR-TAMISEMI Dk Charles Msonde amesema  TAMISEMI kama watendaji katika ngazi za mikoa na serikali za mitaa wataendelea kutoa ushirikiano kwa mashirika yanayoendelea kusaidia katika kuboresha masuala mbalimbali ikiwemo elimu nchini.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo wa Ubalozi wa Uingereza hapa nchini, Kemi Williams ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano walionesha katika kuhakisha magari hayo yananunuliwa ili kwenda kusaidia katika utekelezaji wa Programu ya Shule Bora utakaosaidia maboresho katika Sekta ya elimu nchini kupitia ufuatiliaji na tamthimini.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dk  Aneth Komba amesema TET kama watekelezaji wa mradi wa shule bora kupitia mafunzo tayari, imetoa mafunzo kwa walimu na viongozi mbalimbali wa elimu  nchini yakiwemo ya mbinu za ufundishaji na ujifunzaji zinazozingatia ujumuishi wa walimu.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Angila
Angila
18 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online.(Q) Get this today by follow instructions
.
.
On This Website……………..> > http://remarkableincome09.blogspot.com

MichelleBearden
MichelleBearden
18 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 18 days ago by MichelleBearden
FILI PO
FILI PO
17 days ago

Thanks for the info, just started this 4 weeks ago. I’ve got my FIRST check total of $350, pretty cooll.!

Work At Home Special Report! (financereports.online)

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x